0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

ZAKA ZA MADINI NA HAZINA ILIYOZIKWA ARDHINI

SOMO LA FIQHI

Suali: Madini ni nini? na inamanisha nini ya Hazina iliyozikwa ardhini?

Jawabu: Madini ni chochote kinachotolewa ndani ya ardhi ambacho kwamba sio sampuli ya ardhi kama vile dhahabu, fedha, vyuma, na vijiwe vya tunu kama vile almasi na rubi, na risasi, na vyenginevyo katika vitu asili vinavyotolewa ndani ya Ardhi.

Hazina iliyozikwa ardhini
Ni Mali iliyozikwa ndani ya ardhi kwa kuekwa na mtu, kutokana na dhahabu, na fedha, na mfano wa vitu hivi.

Suala: Ni ipi Hukumu ya zaka ya madini na hazina iliyozikwa ardhini
Jawabu: Hukmu yake ni lazima, kwa kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَنفِقُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا كَسَبْتُمْ وَمِمَّا أَخْرَجْنَا لَكُم مِّنَ الْأَرْضِ}   البقرة:267}

[Enyi mlioamini! Toeni katika vile vizuri mlivyovichuma, na katika vile tulivyokutoleeni katika ardhi] [Al-Baqarah: 267]

Na kauli ya Mtume :

[وفي الركاز الخمس]  رواه البخاري ومسلم

[Na katika hazina iliyozikwa ardhini (toeni) khumusi (1/5))]   [Imepokewa na Bukharin a Muslim.]

Sauli: Ni yapi Masharti ya kutoa zaka ya hazina iliyozikwa ardhini
Jawabu: Hakuna masharti yoyote ya zaka ya hazina iliyozikwa ardhini, basi atakapomiliki mtu hio hazina iliyozikwa ardhini anafaa kutoa zaka yake moja kwa moja.

Kiwango cha kuwajibika mtu kutoa zaka ya madini na hazina iliyozikwa ardhini
Ni wajibu mtu kutoa khumusu (1/5) kwa kichache au kingi atakachopata katika madini na hazina iliyozikwa ardhini, kwa jumla ya kauli ya Mtume ﷺ:

[وفي الركاز الخمس]  رواه البخاري ومسلم

[Na katika hazina iliyozikwa ardhini (toeni) khumusi]     [Imepokewa na Bukhari na Muslim.]


Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.