0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

VIPIMO VYA MALEZI

VIPIMO VYA MALEZI

Malezi ni nguzo na silaha muhimu sana katika jamii yetu.Hivyo basi tunahitaji vipimo vya malezi ili tuweze kufahamu mwelekeo wa sawa katika malezi yetu. Pasi na kuwa na vipimo hatuwezi kujuwa dira na usawa upo wapi. Je tupo katika njia ilio nyoka ama pana udhaifu? Na kama tumetoka katika dira ya sawa sisi sote tunahitaji kujipima mara kwa mara ili tufahamu kama kweli tumechukuwa mwelekeo wa sawa katika maisha yetu.

Kwa hivyo vipimo tutakavyoviweka ni juhudi za kibinadamu lazima vitakuwa na kasoro zake.Unapoona kasoro yoyote tafadhali tufahamishe ili tujuwe ni wapi pa kurekebisha na malipo yako kwa Mola.
Kipimo cha kwanza ni vipi tutataamaliana na Qurani mwongozo wa maisha yetu? Je mtu afanya mambo yafuatayo?
1-Asoma Qurani kila siku?
2-Ahifadhi kiasi kikubwa?
3-Afahamu maana yake?
4-Azingatia na kufikiria?
5-Aitumia katika maisha yake?
6- Aitukuza Qurani?
7-Ajipamba na adabu za Qurani?
Haya mambo saba ni kipimo cha kila mmoja wetu akitaka kujuwa kuwa malezi yake na watu wa nyumbani kwake wapo katika sawa,basi jipime kwa mizani ya mambo hayo saba.

Mizani ya pili ni hizi hatua saba za sunna za mtume Muhammad (S.A.W).Je watekeleza mambo yafuatayo?
1- Je wasoma hadithi?
2- Je wahifadhi kiasi gani cha hadithi?
3- Je wafahamu maana yake?
4- Je wazizingatia na kuzifikiria?
5- Je wazitumia katika maisha yako?
6- Je waheshimu na kutukuza maneno ya mtume?
7- Je wajipamba na sunna za mtume katika maisha yako?
Kipimo cha tatu kwenye mizani yetu ni je unayo elimu ya kisheria ya kukidhi mahitaji yako ya kimaisha?kwa maana hiyo je una kiwango kizuri cha maarifa au una hima ya kutafuta elimu ya kisheria? Wajua fani za ahkam za ibaada na miamala?Je wajuwa mwongozo wa mtume (S.A.W)?Je una angalau utangulizi muhimu wa fani za kidini kama Tawhid, Hadithi,Sera ya mtume(S.A.W) na fiqhi?Je unaweza kutaamiliana na vitabu vya hadithi na Usulul-Fiqhi? Ukipata majibu ya maswali haya tayari utakuwa umejipima kutumia kipimo cha tatu.
Kipimo cha nne ni kujiuliza je una ufahamu wa kisawa wa ni nani Ahli sunna waa jama’a ?(Wenye kushikamana na sunna na umoja).Mtu Ahli sunna wa jama’a ana sifa zifuatazo;
1 –Anamwabudu Allah pekee yake wala hamshirikishi.
2-Anamfuata mtume (S.A.W) wala haleti uzushi katika dini.
3-Ampenda Mola na mtume wake (S.A.W) kushinda wengine.
4-Aweka mizani baina ya khofu na kutarajia malipo ya ALLAH.
5- Apenda kwa ajili ya Allah na anachukia kwa ajili yake.
6- Anamtukuza Mola wake kila wakati.
7- Anajizatiti sana katika masuala ya tawhidi.
Mizani nyingine ya tano ni ya tabia njema.Je mambo yafuatayo yanapatikana katika malezi ya mtoto wako ?
1- Awe ni mtu anayejipamba na tabia njema .
2- Awe mtu anayeiga tabia za mtume(S.A.W) katika maisha yake.
3- Awe mwenye kuheshimu wazazi wake.
4- Awe mwenye kuheshimu watu wengine wakubwa kwa wadogo
5- Awe ni mwenye kujipamba na adabu za kusema.
6- Awe ni mwenye kujipamba na sifa nzuri.
7- Awe mwenye kujiepusha na tabia mbaya

Mizani nyingine ya tano ni yakufikiria namna yakukuza maarifa ya mtu.Mambo yafuatayo ni ya kuzingatiwa
1-Mtu atumie akili yake vyema pasi na kuishughulisha na upuuzi
2-Mtu akuze maarifa yake mara kwa mara kwa sababu mambo mengi ynavumbuliwa kila siku.
3-Mtu aweze kufanya utafiti wa kielimu kwa sababu yako mengi ambayo yanahitaji masuluhisho.
4-Mtu awe na uhodari wa kufafanuwa mambo kwa uzuri
5-Mtu awe na uhodari wa kuvumbua mambo
6-Mtu ajuwe kutumia vifa vya kileo kama ngamizi (tarakilishi) n.k
7-Mtu aendelee na kuboresha maarifa yake

Mizani nyingine ya saba muhimu ni mizani ya daawah.Katika kufanya daawah mambo yafuatayo ni muhimu sana mtu ayazingatie;
1- Je wafanya daawah?
2- Je wahisi daawah ni jukumu lako?
3- Je wajipamba na sifa za daiyaah?(mwenye kufanya daawah)
4- Je wafuata nyayo za mtume katika dawaah?
5- Je waamrisha mazuri na kukataza mabaya?
6- Je una uhodari wakukinaisha mtu na kumuathiri?
7- Je unaweza kuiendesha idara ya mambo ya daawah ?
Tujipime kwa mizani ya haya tuliyoyaeleza ili tuweze kufahamu kama tupo katika njia iliyonyooka katika malezi yetu na jamii yetu kwa ujumla.
JAZAKALLAH KHEIR

Makala yanaendelea….

Imeandika na Sheikh Abuu Hamza

Mombasa-Kenya.

Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.