0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

FADHILA ZA ADHANA

FADHILA ZA ADHANA

Zimepokelewa hadithi kadhaa kutoka kwa Mtume wa Allah  zinazofahamisha fadhila na thawabu kubwa zinazopatikana ndani ya adhana.

Miongoni mwa hadithi hizo ni kama zifuatavyo:

1. Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah  radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu  amesema:

[لو يعلم الناس ما في النداء والصف الأول ثم لم يجدوا إلا أن يستهموا عليه لاستهموا]      رواه البخاري ومسلم

[Lau watu wangelijua yaliyomo katika wito (adhana) na safu ya kwanza (ya swala ya jamaa) Kisha wasipate (fursa hizo) ila kwa kupiga kura, basi wangelipiga kura.]    [Imepokewa na Bukhaari na Muslim]

2. Imepokelewa kutoka kwa Abuu Said Al-khudriy  Radhi za Allah ziwe juu yake  amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ :

إني أراك تحب الغنم والبادية، فإذا كنت في غنمك وباديتك فأذنت بالصلاة، فارفع صوتك بالنداء، فإنه لا يسمع مدى صوت المؤذن جن، ولا إنس، ولا شيء، إلا شهد له يوم القيامة      رواه البخاري

[Mimi nakuona unapenda (kuchunga) mbuzi na kukaa Baadiya (majangwani) utakapokuwa Badia na mbuzi wako ukaadhini kwa ajili ya Swala Basi inyanyue sauti yako kwa wito huo (adhana) kwani hakika haisikii sauti ya muadhini jini wala mwanadamu wala kitu cho chote ila (sauti hiyo) itamshuhudia siku ya kiyama.]     [Imepokewa na Bukhari]

3. Mtume wa Mwenyezi Mungu  amewaombe Mungu wenye kuadhini na akaomba kwa kusema:

[اللَّهُمَّ أَرْشِدِ الْأَئِمَّةَ، وَاغْفِرْ لِلْمُؤَذِّنِينَ]   اخرجه أبوداود وصححه الألباني

[Ewe Mwenyzi Mungu waongoze maimamu na na uwasamehe wenye kuadhini]                [Imepokewa na Abuu Dawud na kusahihishwa na Al Baaniy]


Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.