0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

WAJIBU ZA HIJJA

SOMO LA FIQHI

Wajibu za Hijja
1. Kuhirimia kwenye sehemu zilizowekwa kuhirimia:
kwa neno lake ﷺ baada ya kuzitaja sehemu za kuhirimia:

[هُنَّ لَهُنَّ، وَلِمَنْ أَتَى عَلَيْهِنَّ مِنْ غَيْرِهِنَّ مِمَّنْ أَرَادَ الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ]    رواه البخاري

[Hizo ni za watu wa sehemu hizo na wale wanaokuja hapo kati ya watu wa sehemu nyingine miongoni mwa wale wanataka kuhiji au kufanya Umrah]   [Imepokewa na Bukhari].

2. Kusimama Arafa mpaka jua kuzama kwa aliyesimama mchana:
Kwa kuwa Mtume ﷺ alisimama mpaka jua likazama.

3. Kulala hapo Muzdalifa:
kwa sababu Mtume ﷺ alilala hapo na akasema:

[لِتَأْخُذْ أُمَّتِي نُسُكَهَا، فَإِنِّي لَا أَدْرِي لَعَلِّي لَا أَلْقَاهُمْ بَعْدَ عَامِي هَذَا]   رواه ابن ماجه

[Umma wangu wachukue ibada yao ya Hija kutoka kwangu, kwani mimi sijui pengine huenda nisikutane nao baada ya mwaka wangu huu]   [Imepokewa na Ibnu Maja.]

Na kwamba yeye ﷺ aliwaruhusu Waislamu madhaifu baada ya nusu ya usiku. Hilo linaonyesha kwamba kulala hapo Muzdalifa ni lazima. Na Mwenyezi Mungu Ameamrisha atajwe katika Mash’ar al-Haraam.

4. Kulala Mina masiku ya siku za Tashriiq:
kwa ilivyothubutu kwamba Mtume  aliwaruhusu wachungaji kulala kando ya Mina [Imepokewa na Abu Yalaa katika Musnad yake.].

Hii inaonyesha kwamba asili ni kuwa kulala Mina ni wajibu.

5. Kuvirushia viguzo vijiwe,
kwa kauli Yake Aliyetukuka:

{ وَٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ فِيٓ أَيَّامٖ مَّعۡدُودَٰتٖۚ } البقرة: 203

[Na mtajeni Mwenyezi Mungu katika siku zinazohesabika]   [2: 203].

Na siku zinazohesabika: ni siku za ashriiq.

Na kurusha vijiwe ni miongoni mwa kumtaja Mwenyezi Mungu, kwa neno la Mtume (saw):

[إِنَّمَا جُعِلَ الطَّوَافُ بِالْبَيْتِ وَبَيْنَ الصَّفَا والْمَرْوَةِ وَرَمْيُ الْجِمَارِ لِإِقَامَةِ ذِكْرِ اللهِ]   رواه أبو داود

[Hakika kutufu Alkaba, kusai baina ya Swafaa na Marwah na kuvirushia viguzo vijiwe ni miongoni mwa kusimamisha utajo wa Mwenyezi Mungu]   [Imepokewa na Abu Daud.].

6. Kunyoa au kupunguza,
kwa neno la Mwenyezi Mungu Aliyetukuka:

{لَتَدۡخُلُنَّ ٱلۡمَسۡجِدَ ٱلۡحَرَامَ إِن شَآءَ ٱللَّهُ ءَامِنِينَ مُحَلِّقِينَ رُءُوسَكُمۡ وَمُقَصِّرِينَ}  الفتح: 27

[Mtaingia Msikiti wa Haram mkiwa kwenye amani, Mwenyezi Mungu Atakapo, hali ya kunyoa vichwa vyenu na kupunguza]   [48: 27].

7. Kutufu twawafu ya kuaga:
kwa haditi iliyothubutu kutoka kwa Ibnu ‘Abbas Radhi za Allah zimfikie yeye kuwa alisema:

[أُمِرَ النَّاسُ أَنْ يَكُونَ آخِرُ عَهْدِهِمْ بالبيت، إِلَّا أَنَّهُ خُفِّفَ عَنِ الْحَائِضِ]     رواه مسلم

[Wameamrishwa watu kuwe kule kutufu twawafu ya kuaga iwe shughuli yao ya mwisho kwenye Alkaba, isipokuwa mwenye hedhi alirahisishiwa]    [Imepokewa na Muslim].

Tanbihi

Wajibu wa Hajji
Mwenye kuacha wajibu itamlazimu kuchinja mnyama ili kuunga upungufu huu.


Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.