0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

WAISALMU NA QADHIA YA MASJIDUL AQSWA

WAISALMU NA QADHIA YA MASJIDUL AQSWA

Kadhia ya msikiti mtukufu wa masjidul Aqswa ni kadhia ya kila muislamu ulimwenguni wala si kadhia ya waarabu na waisraeli wala wapalestina na mayahudi kama waislamu wengi wanavyodhania kwa sababu ya kutojua umuhimu wa msikiti wa Aqswa katika Uislamu.
Msikiti wa Aqswa ulioko katika mji wa Qudsi ni Kibla cha kwanza cha waislamu na ni haram ya tatu takatifu,na ni katika misikiti mitatu ambayo anaruhusiwa muislamu kufunga safari kwa ajili ya kuyazuru. Mtume MUHAMMAD ﷺ amesema:

[لا تشد الرحال إلا إلى ثلاث مساجد المسجد الحرام ومسجدي هذا والمسجد الأقصى]     رواه البخاري ومسلم

[Haifungwi safari (kwa ajili ya ziara) ila kwenda katika misikiti mitatu Masjidul Haram na Msikiti wangu huu na Masjidul Aqswaa]      [Imepokewa na Bukhari na Muslim]

Na Mtume wetu ﷺ kama tunavyo jua alipo pelekwa miraji safari yake aliianzia masjidul Aqswa baada ya kutoka Makkah kisha kupelekwa mbinguni,Mwenyezi Mungu anasema:

{سُبْحَانَ الَّذِي أَسْرَىٰ بِعَبْدِهِ لَيْلًا مِّنَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ إِلَى الْمَسْجِدِ الْأَقْصَى الَّذِي بَارَكْنَا حَوْلَهُ لِنُرِيَهُ مِنْ آيَاتِنَا ۚ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ}

[SUBHANA, Ametakasika aliye mchukua mja wake usiku mmoja kutoka Msikiti Mtukufu mpaka Msikiti wa Mbali, ambao tumevibariki vilivyo uzunguka, ili tumuonyeshe baadhi ya Ishara zetu. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia na Mwenye kuona.]     [Al israa:1]

Aya hii inaonesha wazi mafungamano ya misikiti hii miwili, Mwenyezi Mungu alikuwa anaweza kumpaleka Mtume wake ﷺ kutoka makkah moja kwa moja hadi mbinguni lakini kwanza alimpeleka masjidul Aqswa na huku nikuonyesha wazi kuwa msikiti huu ni miongoni mwa misikiti muhimu kwa waislamu.

Na Mwenyezi Mungu alipowa faradhia waislamu kuswali Swala tano kwa kila siku waislamu walikua wakiswali kuelekea masjidul Aqswa kwa mda wa miezi 16 mpaka mwenyezi mungu alipo muamrisha mtume MUHAMMAD ﷺ kuelekea upande wa msikiti wa Makkah,kwa hivyo msikti huu ndicho kibla cha kwanza kwa waislamu.

KUKOMBOLEWA MASJIDUL AQSWAA.

Alipo shikilia Ukhalifa Umar Ibnul Khatab radhi za Allah ziwe juu yake alimpa uongozi wa kwenda kuikomboa miji ya Shaam Swahaba Mtukufu Abuu Ubayda Aamir Ibnul Jarraah badala ya Khalid Ibnul Waleed radhi za Allah ziwe juu yao, na jeshi likaelekea kwenda kuukomboa mji wa Quds ambao ulikua ukiitwa (Alyaa), alipofika katika mji huo na kupambana na warumi ambao ndio waliokuwa wakiutawala mji huo katika zama hizo,wakashindwa kuingia kwa sababu ya kujihami watu wake katika ngome madhbuti ambazo walikua ndani yake,waislamu wakawazunguka na kuwazingira kwa mda,mpaka walipotaka suluhu na waislamu na wakashurutisha ni lazima aje khalifa wa Wailsamu achukuwe funguo za mji huo,ndipo alipofunga safari Amirul Mu’minina Umar Ibnul Khatwab kutoka Madina hadi katika mji wa Quds na kuchukuwa fungua za mji huo na akaingia katika msikiti huu mtukufu na kachukuwa ahadi kuwapa Amani wakazi wa mji huo na kuandika ahadi hiyo iliyojulikana kama (Al’ahdul Umariyya) na hayo yalitokea katika mwaka wa 15 Hijriyya sawa na mwa wa 636 miladia,na ukabaki msikiti huo katika mikono ya Waislamu mpaka katika vita vya msalaba ambavyo wazungu walikuja na kuuteka tena mji huo wa Quds kwa mara ya pili mwaka wa 1099 miladia na kuuvunja msikiti huo wa Aqswa na kuujenga vingine na kuuita (Haykal Sulayman),mpaka katika mwaka 1187 ndipo waislamu walipoandaa jeshi liliongozwa na Swalahuddin Al Ayyubiy na kuuzingira mji huo na kisha kuukomboa kutoka katika mikono ya wakiristo na kubaki katika mikono ya Wailsamu mpaka ilipokuja dola ya kizayuni dola ambayo iliwekwa na wazungu na kuwaondosha na kuwafukuza wenyeji wapalestina na badala yake kuwaleta Mayahudi kutoka nchi mbali mbali na kuwaweka katika miji hiyo Mwaka wa 1948, na katika mwaka 1967 kulipotokea vita baina ya dola za Kiarabu na Israel ulivamiwa mji wa Qudsi na kubaki chini ya utawala wa Israel hadi leo.

Tanabahisho.

Jambo la kusikitisha ni kuwa waislamu wengi hawajui historia ya msikiti huu mtukufu kwa sababu vijana wetu hawafundishwi historia kama hizi katika mashule wanayosoma kwa lengo la kuwafanya waislamu wasiijue historia na tarehe ya msikiti kama huu,badala yake vijana wetu wanafundishwa historia ya watu wasiokua na maana , na waislamu wengi wanona yakwamba kadhia ya masjidul Aqswa haiwahusu bali ni kadhia ya Waarabu na Israel na hivi ndivyo wanavyotaka makafiri ili waislamu wasijihusishe kabisa na kadhia kama hii, na sasa hivi mayahudi wanaenda mbio kuifanya kadhia hii iwe ni kadhia ya wapalestina na mayahudi , na pia waarabu wajitoe na wabaki wapalestina peke yao lakini ukweli wa mambo ni kuwa kadhia kama hii inawahusu waislamu wote duniani na ni wajibu wa kila muislamu kuuhami na kuulinda msikiti wa Aqswa ,na watakapo acha kuuhami msikiti huu basi watakwenda kuulizwa na Mwenyezi Mungu siku ya kiyama.

Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.