0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

UONGOZI- Dr. Majid Hobeni

UONGOZI

Nidhamira ya uandishi huu kuangazia suala la uongozi ambalo ni sehemu  muhimu katika maisha ya binadamu na hata viumbe vengine.
Uongozi dufu au mbaya ni chanzo cha upotofu wa dini,Dunia na Akhera pia.
Tutachukua kiegezo kwa MUSA (Alayhi salam) kwa sababu ni mmoja katika mitume walotumwa kupambana na udhalimu, unyanyasaji, maonevu na ubaguzi.

MUSA

Musa ibnu Imran mjukuu wa mtume Yaakub (Alayhi salam) alizaliwa Misri wakati wa Firaaun dhalimu ambaye alijulikana kwa maonevu dhulma mauaji, ubaguzi na dhulma nyingi nyingine. Soma Quran Qaswas Aya (4).Mwenyezi Mungu anasema:

{إِنَّ فِرْعَوْنَ عَلَا فِي الْأَرْضِ وَجَعَلَ أَهْلَهَا شِيَعًا يَسْتَضْعِفُ طَائِفَةً مِّنْهُمْ يُذَبِّحُ أَبْنَاءَهُمْ وَيَسْتَحْيِي نِسَاءَهُمْ ۚ إِنَّهُ كَانَ مِنَ الْمُفْسِدِينَ}

[Hakika Firauni alitakabari katika nchi, na akawagawa wananchi makundi mbali mbali. Akalidhoofisha taifa moja miongoni mwao, akiwachinja watoto wao wanaume na akiwaacha watoto wao wanawake. Hakika yeye alikuwa katika mafisadi.]

Musa alijulikana kwa nguvu zake za kimwili na ukaribu wake kwa Allah kwa kuzungumza na Allah mpaka kuomba kutaka kumuona Allah. Soma Quran. Suratul A’raaf Aya (143)

{وَلَمَّا جَاءَ مُوسَىٰ لِمِيقَاتِنَا وَكَلَّمَهُ رَبُّهُ قَالَ رَبِّ أَرِنِي أَنظُرْ إِلَيْكَ ۚ قَالَ لَن تَرَانِي وَلَٰكِنِ انظُرْ إِلَى الْجَبَلِ فَإِنِ اسْتَقَرَّ مَكَانَهُ فَسَوْفَ تَرَانِي}

[Na alipo kuja Musa kwenye miadi yetu, na Mola wake Mlezi akamsemeza, alisema: Mola wangu Mlezi! Nionyeshe nikutazame. Mwenyezi Mungu akasema: Hutoniona. Lakini utazame huo mlima. Ukibaki pahala pake basi utaniona].

Tutaangazia kwa Mada hii ya Musa na uongozi dhalimu vipengee vifuatavyo.
(1) kuzaliwa kwa Musa (A.S)
(2) Bahari
(3) kunyonyesha
(4) kahama kwa musa
(5) kuowa kwa musa
(6) Musa akiwa Madyan
(7) Kuajiriwa kwa musa
(8) Musa kurudi Misri
(9) Musa Kupewa Risala (UTUME ) njiani
Kufikia hapa tutakuwa tumejaribu kueleza maisha ya mwanzo ya Musa (A.S) na mafunzo alopata kupambana na udhalimu na uongozi mbaya.
Kifungu cha pili tutaangazia
(10) Musa kukumbushwa alivyofadhiliwa au kulelewa na Firaaun
(11) Banuu Israel Misri
(12) Uchoyo /au kujipenda zaidi
(13) Kutafuta mustaqbal mzuri
(14) Kujifunza kwa khidri
(15) Musa /wachawi
(16) Siku ya idd
(17) Musa kuomba apewe nduguye amsaidie.
(18) Vishawishi au visaidizi alokuwa nazo musa
(19) Utawala / utajiri
(20) Hasira ya Firaaun
(21) Kukimbia kwa Musa
(22) Bahari mara ya pili
(23) Kuangamizwa udhalimu
Kufikia hapa tutakuwa tumejaribu kuangazia mapambano ya musa na Utawala mbaya au uongozi dhalimu, tutaanza kuangazia Utawala wa Musa (A.S)
(24) Watu wa musa na mazowea ya upotofu

(25) Tabia yakupenda mali (Qaruun)
(26) Musa kuenda kuonana na Allah ( kuzungumza )
(27) Samiriyu – Upotofu kwa Utawala wa Musa
(28) Haroun kuogopa Fitna
(29) Kijigombe – Mungu mpya kwa Utawala wa musa (upotofu)
(30) Musa kupewa sheria ya serekali yake
(31) Hasira Takatifu
(32) Kujitetea
(34) Vita juu ya upotofu wa samiriyu

(35) Vita juu ya utukufu wa Utajiri  (Qaruun)
(36) Musa na Ardhi takatifu
(37) kufa kwa Haroun
(38) kufa kwa Musa
(39) Mafunzo (1)
(40) Mazingatio/ Mwisho

Imeandikwa na Dr.Majid Hobeni

Deputy principal  College of Islamic studies mombasa

Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.