0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

MNYAMA WA UDH’HIYA NA HUKMU YAKE

SOMO LA FIQHI

Maana ya mnyama wa Udh’hiya

Ni yule anayechinjwa miongoni mwa wanyama howa siku za idd ya kuchinja kwa kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka.

Hukumu ya kudhahi
Ni sunna iliyotiliwa mkazo, kwa neno lake Mwenyezi Mungu Aliyetukuka:

{فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَٱنۡحَرۡ}   الكوثر: 2

[Basi mswalie Mola wako na uchinje]   [108: 20].

Na kwa Hadithi ya Anas Radhi za Allah ziwe juu yake:

[ أن النبي ﷺ ضَحَّى بِكَبْشَيْنِ أَمْلَحَيْنِ ، ذَبَحَهُمَا بِيَدِهِ، وَسَمَّى وَكَبَّرَ، وَوَضَعَ رِجْلَهُ عَلَى صِفَاحِهِمَا]   رواه الترمذي

[Kwamba Mtume ﷺ alidhahi (alichinja) kondoo wawili wazuri  [ Amlah: Mnyama mwenye weupe na weusi, na weupe ukawa ni mwingi zaidi.] wenye pembe  Aliwachinja kwa mkono wake. Akapiga bismillahi na akaleta takbiri na akaweka guu lake juu mbavu zao]             [Imepokewa na Tirmidhi].

Wakati wa kuchinja mnyama wa Udh’hiya

Wakati wa kuchinja unaanza baada ya Swala ya Idd ya kuchinga mpaka jua la siku ya mwisho wa siku za Tashriiq kuzama (Siku ya kumi na moja, kumi nambili na kumi na tatu za mwezi wa Mfungotatu).

Mnyama wa Udh’hiya anayetosheleza
1. Mbuzi au kondoo mmoja anamtosheleza mtu mmoja. Na anaweza kumshirikisha anayemtaka katika thawabu, kwa kuwa Mtume alipotaka kuchinja mnyama wake wa kudhahi alisema:

[بِاسْمِ اللهِ، اللَّهُمَّ تَقَبَّلْ مِنْ مُحَمَّدٍ، وَآلِ مُحَمَّدٍ، وَمِنْ أُمَّةِ مُحَمَّدٍ]    متفق عليه

[Bismillahi. Ewe Mola mtakabalie Muhammad na jamaa za Muhammad na umma wa Muhammad]    [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

2. Ngamia mmoja na Ng’ombe mmoja wanawatosheleza watu saba.  Yafaa kwa watu saba kushirikiana katika Ngamia au Ng’ombe, kwa kauli ya Jabir:

[ فَأَمَرَنَا رَسُولُ اللهِ ﷺ أَنْ نَشْتَرِكَ فِي الإِبِلِ وَالْبَقَرِ، كُلُّ سَبْعَةٍ مِنَّا فِي بَدَنَةٍ ( البدنة: هي الناقة، ذكرا كانت أو أنثى) ].   رواه مسلم

[Akatuamrisha Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ tushirikiane katika ngamia na ng’ombe, kila watu saba miongoni mwetu kwa ngamia mmoja (Badanah: ni ngamia, awe ni mwanamke au mwanamke.) ]    [Imepokewa na Muslim.].

Miaka ya mnyama inayotosheleza kwa Udh’hiya

Jadha› wa kondoo: Naye ni mwenye miezi sita.

Thanii wa mbuzi: ni mwenye mwaka mmoja.

Thanii wa ng’ombe: ni mwenye miaka miwili.

Thanii wa ngamia: ni mwenye miaka mitano.

Mnyama bora wa Udh’hiya
Mnyama bora ni ngamia ikiwa atatolewa mzima kwa sababu thamani yake iko juu na nimanufaa kwa mafakiri kisha ni Ngo;mbe ikiwa atatolewa mzima kisha Mbuzi, kisha fungu la saba la Ngamia kisha fungu la saba la Ngo’mbe

Aibu za mnyama wa Udh’hiya
1. Aibu zinazozuia kutosheleza [Inazuilia kutosheleza: Haisihi kumchinja kama mnyama wa kudhahi.]
‹Awraa’›: Ni mnyama mwenye ila machoni mwake, na anaingia ndani ya huyo mnyama kipofu.

‹Arjaa›: Ni mnyama asiyeweza kutembea.

‹Ajfaa’›: Ni mnyama aliyekonda asiye na mafuta.

Mgonjwa ambaye ugonjwa wake uko wazi:

Dalili ya hayo ni Hadithi iliyopokewa na Baraa bin Aazib Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ alisema:

لَا يَجُوزُ مِنَ الضَّحَايَا الْعَوْرَاءُ الْبَيِّنُ عَوَرُهَا، وَالْعَرْجَاءُ الْبَيِّنُ عَرَجُهَا، وَالْمَرِيضَةُ الْبَيِّنُ مَرَضُهَا، وَالْعَجْفَاءُ الَّتِي لَا تُنْقِي [ لا تنقي: أي ليس فيها مخ]ِ   . رواه مسلم

[Haifai kudhahi kwa mnyama mwenye jicho moja ambaye kasoro katika jicho lake iko wazi, na mnyama kiguru ambaye kiguru chake kiko wazi, na mngonjwa ambaye ugonjwa wake uko wazi, na aliyekonda asiye na mafuta   [ Laa tanqii: hana bongo.] ]  [Imepokewa na Muslim.]

Na zinakutanishwa na hizi, aibu ambazo hufanana na hizi au ni mbaya zaidi kuliko hizi.

2. Aibu zisizozuia kutosheleza kudhahi
AL-Batraa›: Asiye na mkia.

AL-Jammaa›: asiye na pembe kimaumbile.

AL-Khaswiyy: Kondoo ailiyekatwa konde zake za dhakari.

Alie na mpasuko kwenye sikio lake au tundu, au pembe yake imevunjika.

Haya yaliyotajwa kuhusu kinachotosheleza katika kudhahi ndiyo hayo hayo kuhusu tunuku na fidia.

Kugawanya nyama ya Udh’hiya
Imeruhusiwa na sharia kwa mwenye kudhahi ale theluthi ya nyama yake, na akiitoa sadaka yote inafaa, na akila nyingi ya ile nyama pia inafaa.

Faida
Mwenye kutaka kudhahi, haifai akate nywele zake na kucha zake na kitu chochote mwilini mwake ungiapo mwezi wa Mfungotatu mapaka achinje. Hii ni kwa hadithi iliyopokewa na Ummu Salama Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ alisema:

[إِذَا دَخَلَتِ الْعَشْرُ وَأَرَادَ أَحَدُكُمْ أَنْ يُضَحِّىَ فَلاَ يَمَسَّ مِنْ شَعَرِهِ وَبَشَرِهِ شَيْئًا].  رواه مسلم

[Zinapoingia Siku kumi (za mwezi wa mfungo tatu) na akataka mmoja wenu kudhahi, basi asiondowe chochote katika nywele zake na mwili wake]   [Imepokewa na Muslim.].

Ama wale ambao wanafanyiwa tendo la kudhahi, kama mke na watoto, si haramu kwao kuondoa nywele au uchafu wa mwilini kama kucha.

Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.