0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

IDUL-FITR

IDUL-FITR

Iddi ya Fitri ni Iddi ya kwanza kwa Waislamu. Waislamu wanasherehekea katika mwezi wa Shawwal kinyume na Iddul adhha ambapo Waislamu wanasherehekea katika mwezi wa Dhulhijjah. Waislamu wanakula baada ya kufunga mwezi mzima, ni haramu kufunga siku hiyo. Na muda wa kusherehekea ni siku moja hadi siku sita.

Shukrani zote ni za Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Taala kukamilisha kufunga mwezi wa Ramadhani. Amesema Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Taala:

شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِي أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَىٰ وَالْفُرْقَانِ ۚ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ ۖ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ ۗ يُرِيدُ اللَّهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُوا الْعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُوا اللَّهَ عَلَىٰ مَا هَدَاكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ

[Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani kuwa ni uwongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi. Basi ataye kuwa mjini katika mwezi huu naafunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika siku nyengine. Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa kuwa amekuongoeni ili mpate kushukuru.]   [Al-Baqara:185]

Amesema ‘Umar Radhi za Allah ziwe juu yake siku mbili hizi Mtume ﷺ amekataa kufunga yaani Iddul-fitr (baada ya mwezi wa Ramadhani) na Idul-Adhha (Baada ya Hajj).

Amepokea Anas Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ alikwenda Madina na walikuwa wana siku mbili za kucheza, Mtume ﷺ akasema:

[إِنَّ اللَّهَ قَدْ أَبْدَلَكُمْ بِهِمَا خَيْرًا مِنْهُمَا ، يَوْمَ الأَضْحَى وَيَوْمَ الْفِطْرِ]    رواه أحمد

[Hakika Mwenyezi Mungu amekubadilishieni siku mbili hizo kwa Iddul-fitr na Iddul Adhha].     [Imepokewa na Ahmad]

Siku ya Iddi ni siku ya mapambo. Imepokewa kwa Ibnu ‘Umar kuwa alinunua juba sokoni akamuuzia Mtume ﷺ kuwa ajipambe nalo siku ya Iddi, Amepokea Anas Ibnu Malik kuwa Mtume Swalla Llahu ‘alayhi wasallam amesema:[Haendi kuswali swala ya Iddul-fitr mpaka ale Tende].

Hukumu ya Utoaji wa Sadaka ya Fitri

Amepokea Ibnu ‘Abbas  Radhi za Allah ziwe juu yake kwa Mtume ﷺ amefaradhisha Zakatul-fitri kumtakasa aliyefunga kutokana na michezo, pia kuwa ni chakula cha maskini. Mwenye kutoa kabla ya swala basi ametoa zaka na atakayetoa baada ya swala basi hio ni sadaka miongoni mwa sadaka.

Kupiga Takbir za Iddi

Asili ya jambo hilo Neno lake Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Taala:

 {وَلِتُكْمِلُوا الْعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُوا اللَّهَ عَلَىٰ مَا هَدَاكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ}      البقرة:185

[Na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa kuwa amekuongoeni ili mpate kushukuru.]   [Al-Baqara:185]

Imepokewa na Ibnu ‘Umar  Radhi za Allah ziwe juu yake akisema kuwa: [Mtume ﷺ alikuwa akipiga Takbiri alipo kwenda kuswali swala ya Iddi].

Sikiliza Mada hii na Sheikh Yusuf Abdi


Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.