0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

DAI LA KUPIGWA BIBI FATIMA (R.A) NA MASWAHABA

DAI LA KUPIGWA BIBI FATIMA(R.A) NA MASWAHABA

Katika shubuhati wanazo dai Mashia kuwa kikundi cha maswahaba kikiongozwa na Sayyidna Umar na Khalid bin Al-waleed radhi za Allah ziwe juu yao walivamia nyuma ya bibi Fatima radhi za Allah ziwe juu yake.

Wakampiga mpaka akaangusha mimba yake na kumvuda mkono wake na kumchomea nyumba yake. Kisha kumtoa Sayyinda Ali (r.a.) kwa nguvu na kumlazimisha kwenda kuumpa (Kumvoti) sayyidna Abubakar (r.a)

Jawabu:

Kwanza hakuna riwaya swahihi ya kisa hiki cha urongo katika vitabu vya Ahlu Sunna vya kutegemewa. Kisa hiki kinaelezewa katika vitabu visio tegemewa vilivyo pokelewa na watu wasio julikana, watu warongo na baadhi wananukuu bila ya kuwa na Isnaad yoyote ile.

Na lau kitasihi kisa hiki basi kitathibitisha jambo baya sana kwa hao wanadai kisa hiki na kuonyesha haya yanayo fuata:

1. Kuutia dowa ushujaa wa Sayyidna Ali (r.a) kwani akijulikana ushujaa wake kama ilivyo kuja kwenye sifa zake,

Vipi ataridhia kwa kupigwa mke wake mpaka kuangusha mimba na kuvunjwa mkono na kuchomewa nyumba bila ya kumtetea?  Tena aliye fanyiwa hivyo ni binti wa mtume wake, na binti ya ibnu Ammi yake.

Kwali hilo la ingia akilini?

Ikiwa mtume amesema :

[ومن قتل دون أهله فهو شهيد]    رواه أحمد

[Mwenye kuuliwa akitetea Ahli yake basi yeye ni Shahid]

[Imepokewa na Ahmad].

Na fadhla hizi ni kwa Muislamu yoyote yule atakae simama kumtetea ahli yake.

Je? Itakuwaje kwa swahaba mtumkufu Sayyidna Ali radhi za Allah ziwe juu yake iwe atamuache mkewe na asimtete hata kama atauliwa juu ya jambo hilo.

Kwa hivyo kisa hicho wanacho kidai Mashia kwanza chamtia doa kwa Imamu wao wa kwanza.

2. Ikiwa mashia watadai kuwa Sayyidna Ali hakuweko pindi alipo pigwa bibi Fatima radhi za Allah ziwe juu yake.

Jawabu:

Hilo pia itakuwa ni kuvunda itikadi yao juu ya Maimamu wao kuwa wanajua mambo ya gheyb.

Vipi imamu Ali asijue tukio hilo na ilhali mwadai kuwa maimamu wanajua mambo yalio fichika? Na hapa ni lazima mukubali moja katika mawili:

1. Ima mukubali kuwa itikadi ya kuamini kuwa mimamu wajua gheyb ni itikadi batili?

2. Ama mukubaki kuwa wajua gheyb na Sayyidna Ali alikuwa ajua tukio hilo la kupigwa kwa bibi yake, na hili itakuwa mwamtuhum Sayyidna Ali kuwa alikuwa muoga?.

Kwa hivyo chaguo ni lenu.

Na kisa hiki kimepingwa na mwanachuoni wa kiishia katika nchi ya Libanon Mahamad Husein fadhlullah.

Subhanallah !!

Mashia wamekibuni kisha hiki kwa kutaka kuwatia doa Maswahaba wa bwana Mtume ﷺ lakini hawakujua kuwa wamtia doa Imamu wao.

3. kisha vipi Sayyidna Ali amuozeshe binti yake Ummu Kalthum mume ambae alimpiga mama yake, na kumchomea nyumaba yake?

Huko ndiko kuhifadhi tangamano la ndoa yake na bibi Fatima (r.a)
Hivi ndivyo wanavyo lipwa madhaimu?

Bila shaka si hivyo wala Sayyinda Ali hakuwa hivyo, bali alikuwa ni shujaa alie kuwa haogopi kufa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.

Yeye ndie fi-dai (Shujaa) wa kwanza katika dini pindi alipo lala katika kitanda cha Mtume siku ya hijra bila ya kujali wala kufikiria
Lakini hiki ni kisha cha kubuniwa na Mashia kwa lengo la kutaka kuwatuhumu maswhaba wa Mtume lakini lengo lao halikutimia.

Ni wale walio potea warudi katika dini ya haki, na wasifuate batili bali waregee katika mafundisho ya Qur’ani tukufu na hadithi za Bwana Mtume ﷺ zilizo sahihi.

Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.