0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

274. Riyadhu Swalihina Mlango wa Kuwafanyia wema Wanawake Hadithi 02

BUSTANI YA WATU WEMA


وعن عبد الله بن زَمْعَةَ – رضي الله عنه -: أنَّهُ سَمِعَ النَّبيّ – صلى الله عليه وسلم – يَخْطُبُ، وَذَكَرَ النَّاقَةَ وَالَّذِي عَقَرَهَا، فَقَالَ رَسُول الله – صلى الله عليه وسلم -: {﴿إِذ انْبَعَثَ أشْقَاهَا﴾ انْبَعَثَ لَهَا رَجُلٌ عَزيزٌ، عَارِمٌ مَنيعٌ في رَهْطِهِ}، ثُمَّ ذَكَرَ النِّسَاءَ، فَوعَظَ فِيهنَّ، فَقَالَ: {يَعْمِدُ أحَدُكُمْ فَيَجْلِدُ امْرَأتَهُ جَلْدَ العَبْدِ فَلَعَلَّهُ يُضَاجِعُهَا مِنْ آخِرِ يَومِهِ} ثُمَّ وَعَظَهُمْ في ضَحِكِهمْ مِنَ الضَّرْطَةِ، وَقالَ: {لِمَ يَضْحَكُ أَحَدُكُمْ مِمَّا يَفْعَلُ؟! }     مُتَّفَقٌ عَلَيهِ


شرح الحديث مع فضيلة الشيخ خالد بن عثمان السبت حفظه الله تعالى



Imepokewa kutoka kwa Abdullâh bin Zam‘ah Radhi za Allah ziwe juu yake amesimulia kuwa alimsikia Mtume akikhutubu, akamtaja ngamia (wa Nabii Swaleh) na aliemchinja. Mtume akasema: [Aliposimama muovu wao mkubwa (ili kumchinja ngamia huyo wa miujiza). Alisimama mtu mwenye iza aliye muovu fisadi mwenye kinga ya watu wake (akamchinja)] Kisha akagusia wanawake, akatoa waadhi kuhusu wao, akasema: [Mmoja wenu anampiga mkewe kama anavyomchapa mtumwa na pengine akalala naye mwisho wa siku hiyo (aliyompiga)] Halafu akawapa mawaidha kuhusiana na kucheka kwao kwa sababu ya kushuta (kujamba), akasema: [Mbona mmoja wenu anacheka kwa jambo analolifanya?]    [Wameafikiana Bukhari na Muslim]

Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.