0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

160. Riyadhu Swalihina Mlango wa kuzihifadhi Sunna na Adabu zake Hadithi ya 05


BUSTANI YA WATU WEMA


رياض الصالحين 


عنْ أَبِي عبدِ اللَّه النُّعْمَانِ بْنِ بَشيِرٍ رضي اللَّه عنهما، قال: سمِعْتُ رسولَ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم يقولُ : « لَتُسَوُّنَّ صُفُوفَكُمْ أَوْ لَيُخَالِفَنَّ اللَّه بَيْنَ وُجُوهِكمْ »   متفقٌ عليه

وفي روايةٍ لِمْسلمٍ : كان رسولُ اللُّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم يُسَوِّي صُفُوفَنَآ حَتَّى كأَنَّمَا يُسَوي بِهَا الْقِداحَ حَتَّى إِذَا رأَى أَنَّا قَدْ عَقَلْنَا عَنْهُ ثُمَّ خَرَجَ يَوماً ، فقامَ حتَّى كَادَ أَنْ يكبِّرَ ، فَرأَى رجُلا بادِياً صدْرُهُ فقالَ : « عِبادَ اللَّه لَتُسوُّنَّ صُفوفَكُمْ أَوْ لَيُخَالِفَنَّ اللَّه بيْن وُجُوهِكُمْ »


Kutoka kwa Abuu ‘Abdillaah, An-Nu’maan bin Bashiyr  Radhi za Allah ziwe juu yake Nilimsikia Mtume akisema: [Wa-Allaahi mtazisawazisha safu zenu au Mwenyezi Mungu Atazibadilisha nyuso zenu]    [Imepokea na Bukhari na Muslim] 

Na katika Riwaya nyingine ya Muslim imesema:

alikuwa Mtume ﷺ  akizisawazisha safu kana kwamba alikuwa anasawazisha kwazo mshale, mpaka alipo tuona tumelifahamu hilo. Kisha siku moja akatoka, akasimama hata alipokaribia kupiga Takbiri, akamuona mtu kifua chake kimetokeza, akasema: [Enyi waja wa Mwenyezi Mungu, mtasawazisha safu zenu au Mwenyezi Mungu Atazibadilisha nyuso zenu]


Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.