0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

NGUZO SITA ZA IMANI

Nguzo za Imani (Arkaan al-Imaan) Nguzo 6 za Imani kwa Mpangilio:

1. Kuamini Mwenyezi Mungu (Allaah)

Ushahidi kutoka katika Qur’an:

” ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡحَيُّ ٱلۡقَيُّومُۚ “

Mwenyezi Mungu! Hapana mungu ila Yeye, Aliye Hai, Msimamizi wa kila kitu…”  [Surat Al-Baqarah](w), 2:255)

Ushahidi kutoka katika Hadith:  Kutoka kwa ‘Umar Radhi za Mwenyeezi Mungu ziwe juu yake ambaye amesema:

 فَأَخْبرني عن الإِيمان. قال: [أَن تُؤمِنَ باللهِ، وملائِكَتِهِ وكُتُبِهِ، ورسُلِهِ، واليَوْمِ الآخِرِ، وتُؤمِنَ بالْقَدَرِ خَيْرِهِ وشَرِّهِ]

Niambie kuhusu Imani. Akasema (Mtume Rehma na amani zimfikie yeye) [Ni kumwamini Mwenyeezi-Mungu, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Mitume Yake na siku ya Qiyaama, na kuamini ya kuwa kheri na shari zinatoka Kwake (Allaah alie tukuka  ]….” (Hadith ndefu ya Jibril, [Sahih Muslim](w))

2. Kuamini Malaika wa Mwenyezi Mungu

Ushahidi kutoka katika Qur’an:“

 بَلۡ عِبَادٞ مُّكۡرَمُونَ لَا يَسۡبِقُونَهُۥ بِٱلۡقَوۡلِ وَهُم بِأَمۡرِهِۦ يَعۡمَلُونَ

Bali hao (wanao waita wana) ni watumwa walio tukuzwa. Hawamtangulii kwa neno, nao wanafanya amri zake.  [ Surat Al-Anbiyaa 21:26-27 ]

Dalili kutoka Hadith:   …na uwaamini Malaika wa Mwenyezi Mungu..   (Hadith ya Jibril – Muslim)

3. Kuamini Vitabu vya Mwenyezi Mungu

Ushahidi kutoka katika Qur’an:

{ نَزَّلَ عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ وَأَنزَلَ ٱلتَّوۡرَىٰةَ وَٱلۡإِنجِيلَ }

Amekuteremshia Kitabu kwa haki, kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake. Na aliteremsha Taurati na Injili .”   [Surat Aal Imran, 3:3]

Ushahidi kutoka katika Hadith: “…na vitabu Vyake…” (Hadith ya Jibril – Muslim)

4. Kuamini Mitume wa Mwenyezi Mungu

Ushahidi kutoka katika Qur’an:

{ وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا رُسُلٗا مِّن قَبۡلِكَ }

“Hakika Tumewatuma Mitume kabla yako…   [Surat Ghafir 40:78]

Ushahidi kutoka katika Hadith:

…na Mitume Wake…”  (Hadith ya Jibril – Muslim)

5. Kuamini Siku ya Mwisho (Qiyama)

Ushahidi kutoka katika Qur’an:

وَٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ يُؤۡمِنُونَ بِهِۦۖ وَهُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ يُحَافِظُونَ

“Na wenye kuamini Akhera wanakiamini hichi, nao wanazihifadhi Sala zao”   [Surat Al-An’am 6:92]

Ushahidi kutoka katika Hadith:

“…na kuamini Siku ya Mwisho…”  (Hadith ya Jibril – Muslim)

6. Kuamini Qadar (maisha ya kudura) kheri na shari yake

Ushahidi kutoka katika Qur’an:

{ إِنَّا كُلَّ شَيۡءٍ خَلَقۡنَٰهُ بِقَدَرٖ }

“Hakika sisi tumemuumba kila kitu kwa Qadar (kudura). ”     [Surat Al-Qamar 54:49 ]

Ushahidi kutoka katika Hadith:  “…na kuamini Qadar – kheri na shari yake.”  (Hadith ya Jibril – Muslim) —

Hitimisho:

Nguzo hizi sita ndizo msingi wa imani ya Muislamu. Mtu hawezi kuwa na imani sahihi mpaka azikubali zote kwa pamoja.



Begin typing your search above and press return to search.