0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

NGUZO ANO ZA UISLAMU

Nguzo Tano za Uislamu (Arkanul-Islaam)

1. Kushuhudia kuwa hakuna Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah, na kwamba Muhammad ni Mtume Wake.  (Shahada: Laa ilaaha illaLlaah, Muhammadun RasuluLlaah)

Dalili ya Qur’ani:

{شَهِدَ ٱللَّهُ أَنَّهُۥ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ وَأُوْلُواْ ٱلۡعِلۡمِ قَآئِمَۢا بِٱلۡقِسۡطِۚ}

“Mwenyezi Mungu, na Malaika, na wenye ilimu, wameshuhudia kuwa hakika hapana mungu ila Yeye, ndiye Mwenye kusimamisha uadilifu; ”  [Aali ‘Imran 3:18]

Na Dalili ya Hadithi:  Mtume alisema:

[ بُنِيَ الإسْلَامُ علَى خَمْسٍ: شَهَادَةِ أنْ لا إلَهَ إلَّا اللَّهُ وأنَّ مُحَمَّدًا رَسولُ اللَّهِ، وإقَامِ الصَّلَاةِ، وإيتَاءِ الزَّكَاةِ، والحَجِّ، وصَوْمِ رَمَضَانَ ]

“[Uislamu umejengwa kwa nguzo tano:Shahada kuwa hakuna Mola apasaye kuabudiwa isipokuwa Allaah na Muhammad ni Mjumbe wake, kuswali, kutoa Zaka, kuhiji (Makka) na kufunga Ramadhan.]”   [ Imepokelewa na Bukhari na Muslim]

2. Kusimamisha Swala (Sala) Kuswali swala tano kila siku kwa wakati wake.

Dalili ya Qur’ani:

{ وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَۖ إِنَّ ٱلصَّلَوٰةَ تَنۡهَىٰ عَنِ ٱلۡفَحۡشَآءِ وَٱلۡمُنكَرِۗ}

“Simamisha Swala, hakika Swala humzuilia (mtu) na mambo machafu na maovu…”   [Al-Ankabut 29:45]

Dalili ya Hadithi:  Mtume alisema:

“Tofauti kati ya mtu na ukafiri ni kuacha swala.”   [ Imepokewa na Muslim ]

3. Kutoa Zaka  ( Kuwapa mafakiri na wenye haki mali maalum kila mwaka kwa wenye uwezo.

Dalili ya Qur’ani:

{ وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَۚ }

” Na simamisheni Swala na toeni Zaka”    [Al-Baqara 2:110]

Dalili ya Hadithi:

” Na kutoa Zaka…”  [Bukhari na Muslim] (sehemu ya hadithi ya nguzo tano)

4. Funga Mwezi wa Ramadhani (Saumu)  ( Kufunga kuanzia alfajiri hadi machweo kwa mwezi mzima wa Ramadhani.)

Dalili ya Qur’ani:

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡكُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكُمۡ لَعَلَّكُمۡ

“Enyi mlio amini! Mmeandikiwa Saumu, kama waliyo andikiwa walio kuwa kabla yenu ili mpate kuchamngu.”   [Al-Baqara 2:183]

Dalili ya Hadithi:

…na kufunga Ramadhani…   [Bukhari na Muslim]

5. Kuhiji Nyumba Takatifu ya Allah (Hija) Kufanya ibada ya Hija kwa mwenye uwezo angalau mara moja maishani.

Dalili ya Qur’ani:

{ وَلِلَّهِ عَلَى ٱلنَّاسِ حِجُّ ٱلۡبَيۡتِ مَنِ ٱسۡتَطَاعَ إِلَيۡهِ سَبِيلٗاۚ }

“Na kwa ajili ya Mwenyezi Mungu imewajibikia watu wahiji kwenye Nyumba hiyo, kwa yule awezae njia ya kwendea.”   [Aali ‘Imran 3:97]

Dalili ya Hadithi:

…na kuhiji Nyumba Takatifu ya Allah kwa mwenye uwezo.   [Bukhari na Muslim]

Hitimisho:

Nguzo hizi tano ni msingi wa maisha ya Muislamu. Mtu hawezi kuwa Muislamu wa kweli bila kuzifuata. Zinatuongoza katika imani, ibada, maadili na mafanikio ya duniani na akhera.


Begin typing your search above and press return to search.