0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

MUISLAMU NA KUFANYA KAZI

MUISLAMU NA KUFANYA KAZI

Mwenyezi Mungu ameamrisha kutembea katika Ardhi kwa ajili ya kutafuta rizki na akahimiza kuhusu jambo hilo na hilo linadhihirika katika mambo yafwatayo :
1 Mwenyezi Mungu amekataza kuwaomba watu mali madamu Mwanadamu ana uwezo wa kufanya kazi na kupata riziki kwa juhudi zake na kazi yake, na Mtume ﷺ akaeleza yakawmba atakaewaomba watu mali na yeye ana uwezo wa kufanya kazi na kutafuta riziki basi yeye anapoteza hadhi yake mbele ya Mwenyezi Mungu na mbele ya watu akasema Mtume ﷺ :

[لا تزال المسألة بأحدكم، حتى يلقى الله وليس في وجهه مزعة لحم]     رواه البخاري ومسلم

[Hatoacha mmoja wenu kuomba mpaka akutane na mola wake mtukufu na hana katika uso wake nyama]   [Imepokewa na Bukhary 1405 , Muslim 1040]
Na amesema Mtume ﷺ : [Atakaepatwa na matatizo basi akaiepeleka kwa watu matatizo yake hayatatimizwa na atakae yapeleka matatizo yake kwa ALLAH mtukufu basi ALLAH yuko karibu kumtajirisha]    [Ahmad 3869 , Abu dawood 1645].

Kila kazi za halali ni kazi nzuri ambazo hazina aibu ndani yake .

Kila kazi za kutengeneza vitu na za huduma na za kuwekeza ni kazi nzuri zenye heshma hazina aibu ndani yake, madamu zipo ndani ya mpaka wa vitu halali , na imekuja katika sheria yakwamba Manabii walikua wakifanya kazi za halali za watu wao, kama alivyosema Mtume ﷺ :

[مَا بَعَثَ اللَّه نَبِيًّا إِلا رَعَى الْغَنَمَ]    رواه البخاري

[Mwenyezi Mungu hajamtuma mtume isipokua amechunga mbuzi]   [Imepokewa na Bukhary 2143] ,

Na alikua Nabii Zakariyya seremala  [Muslim 2379]

Na hivyo hivyo Manabii wengine pia walikua wakifanya kazi kama hizo .
kwa hivyo Muislamu atakaekua na nia nzuri katika kazi yake, na anataka kujitimizia mahitaji yake na ya familia yake, na kuwatosheleza na kutowahitajia watu, na kuwanufaisha wanaohitaji , basi atapata ujira kwa ajili ya kazi yake na juhudi zake .

haya ndio Mafundisho ya Uislamu wala sio kama wengi wasio kuwa waislamu wanavyodi kuwa Uislamu ni Dini ya Uvivu.

Makala haya yameandikwa na

Muhammad Fadhil El Shirazy Al Kindy

Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.