0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

MASHIA NA ASHURA’A

MASHIA NA ASHURA’A

Siku ya ashuraa ni siku tukufu,kwani ndio siku ambao Mwenyezi Mungu alimwngamiza Fir’aun na kumuokowa nabii Munsa Alayhi salam,siku hii nabii Musa alifunga kumshukru Mwenyzi Mungu aliyetukuka,na Mtume ﷺ akatuhimiza kufunga siku hii ya Ashuraa kama ilivyo kuja kwenye Hadithi:

      عن أبي قتادة رضي اللَّه عنه ، أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: ” صيام يوم عاشوراء، أحتسب على اللَّه أن يكفر السنة التي قبله. “أخرجه مسلم وأبوداود”

Kutoka kwa Abii Qatada radhi za Allah ziwe juu yake Kwamba Mtume ﷺ amesema:[kufunga siku ya ashura’a natarji kwa ALLAH kwamba inafuta madhambi ya mwaka uliyopita]

[Imepokewa na Muslim na Abuu Daud.

Lakini siku hii kwa Mashia wameibadilisha na kuifanya ni siku ya huzuni na kuomboleza,na isitoshe kufanya mambo ambao dini imekataza, kama kujipiga kwa visu na kujikata kwa mapanga,mpaka kupelekea baadhi yao kufariki, kutokamana na majereha,eti wakidai kufanya hivyo ni katika dini.

Menyezi Mungu anasema katika Qur’ani tukufu:

وَلَا تَقْتُلُوا أَنفُسَكُمْ ۚ إِنَّ اللَّهَ كَانَ بِكُمْ رَحِيمًا}   النساء:29}

[Wala msijiuwe. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwarehemuni.]       [Al-Nnisaa:29]

Na Uislamu umekataza watu kuomboleza katika kulia na Mtume asema:

أنا بريء من الصالقة والحالقة والشاقة]  رواه البخاري]

[Mimi niko mbali na anaeomboleza,na Kunyoa nywele,na mwenye kupasuo nguo (wakati wa msiba)]        [Imepokelewa na Bukhari]

Ikiwa kuomboleza kwa maneno ni haramu je mtu kujipigia na kujiumiza?
Na imekuja hadhiti nyingine:

ليس منا من ضرب الخدود ، وشق الجيوب ، ودعا بدعوى الجاهلية ]   رواه البخاري  ومسلم ]

[Si katika sisi atakae jipiga Matavu (wakati anapo patikana na Msiba) na kupasua Mivuko (nguo) na kuita miito ya kijahiliya]     [Imepokewa na Bukhari na Muslim]

Tunaomba wale ndugu zetu walidanganywa au kutoufahamahu ushia watumia akilizi zao na wajiulize, kweli hayo wanayo yafanwya ni katika dini?

Mbona siku hii imekuwa ni siku ya vichekesho na kuweka pingamizi dhini ya Uislamu kwa wale wasio tafautisha baina ya Uislamu na ushia, na kuona kuwa hayawanayo fanywa na Mashia ni mafundisho ya Waislamu.

Ilhali Dini ya Uislamu uko mbali na haya, na imekuja kukataza kufanya mambo kama haya.

Uislamu umekuja kufundisha huruma mpaka kwa wanyama , Leo utona mtu amkata mototo wake na kumwaga damu yake bila huruma kitendo ambacho hata wanyama hawafanyi hivyo, na lakusikitisha ni kudai kitendo hicho kuwa ni katika dini ,ilhali dini ya uislamu iko mbali na kitendo hicho.

Na kudai kufanya hivyo ni kuhuzunika kwa kifo cha Husein radhi za Allah ziwe juu yake.

Kisha twauliza hawa Mashia kwanini mwaomboleza kifo cha Husein peke yake? Kwani ni yeye pekeyake alieuliwa kidhulma? Sibaba yake husein Sayyidna Ali bin Abiitwalib radhi za Allah ziwe juu yake, pia na yeye si aliuwa kidhulma?

Mbona hamuombolezi siku aliyouliwa??

Bila shaka wanayoyafanya Mashia siku hii ya ashuraa iko mbali na mafunzo ya Uislamu, na yote haya wanayoyafanya si katika Uislamu bali ni dini yao Mashia waliyo ibuni.

Twamuomba Mwenyzi Mungu atuthibitishe kwenye haki, na awaongoze wale waliopotea katika njia ya haki.

Ndugu tazama wanao yafanya Mashia siku hii ya Ashuraa kisha ujuilize kweli huu ndio Uislamu?

Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.