0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

JE WAISLAMU WANAABUDU MASHETANI NA MAJINI??

JE WAISLAMU WANAABUDU MASHETANI NA MAJINI??

Kuna mambo mengi ya uongo yanazuliwa Uislamu na Waislamu hata uislamu hauhusiki nayo, na uzushi huu unaenezwa na madui wa Uislamu kwa kujua au kutojua katika makala haya napenda kujibu madai hayo ya uzushi na kuonesha yakwamba mambo hayo yanayozushwa ni uongo mtupu kwa dalili za wazi kutoka kwenye Qur’ani na Hadithi za Bwana Mtume ﷺ
Wanaeneza wasiokua waislamu ya kwamba Waislamu dini yao ni ya Masheitani na ni wachawi najibu uzushi huu kwa kusema Uislamu ni dini ya Mungu kwa wanaadamu na majini na hakuna hata siku moja Waislamu wamewahi kua na mahusiano na majini wala kuwaabudu majini, majini ni Viumbe wa Mungu kama binaadamu wapo wazuri na waovu, na wao pia wameumbwa kwa ajili ya kumuabudu Mwenyezi Mungu kama alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

{وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ}   الذاريات:56

[Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.]    [Adh-dhaariyaat:56]

na Uislamu ni Dini inatolingania Tawheed kumpwekesha Mwenyezi Mungu kwa Ibaada na kwamba hakuna anaefaa kuabudiwa kwa hali ila Mwenyezi Mungu na hii ndio nguzo ya kwanza ya Uislamu, Vipi tena uzuliwe Uislamu kwa jambo hili la kuwa waislamu wanabudu Majini na Mashetani??

na Mwenyezi Mungu ameliweka wazi jambo hilo,na siku ya Kiyama Mwenyezi Mungu atasema:

{أَلَمْ أَعْهَدْ إِلَيْكُمْ يَا بَنِي آدَمَ أَن لَّا تَعْبُدُوا الشَّيْطَانَ ۖ إِنَّهُ لَكُمْ عَدُوٌّ مُّبِينٌ  وَأَنِ اعْبُدُونِي ۚ هَٰذَا صِرَاطٌ مُّسْتَقِيمٌ}

[Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet’ani? Hakika yeye ni adui dhaahiri kwenu.Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.]   [Ya-sin:60-61]

Ama madai ya kuwa Wailsmau wanabudu Shetani, hayo ni madai ambao hayaingi akilini hata kwa Mtoto mdogo.

nikinukuu katika Qur’ani Mwenyezi Mungu Mungu anatuambia katika sura ya 35 aya ya 6

{إِنَّ الشَّيْطَانَ لَكُمْ عَدُوٌّ فَاتَّخِذُوهُ عَدُوًّا ۚ إِنَّمَا يَدْعُو حِزْبَهُ لِيَكُونُوا مِنْ أَصْحَابِ السَّعِيرِ}

[Hakika Shet’ani ni adui yenu, basi mfanyeni kuwa ni adui. Kwani yeye analiita kundi lake liwe katika watu wa Motoni.]

Kwa hivyo sheitani ni adui yetu na wala hatuwezi kumuabudu kiumbe ama kuhusu Waislamu kua wachawi nasema uchawi na uganga katika Uislami ni haramu ni katika Madhambi makubwa mno katika Qur’ani Mwenyezi Mungu anatuambia katika sura ya 2 aya ya 102

{وَاتَّبَعُوا مَا تَتْلُو الشَّيَاطِينُ عَلَىٰ مُلْكِ سُلَيْمَانَ ۖ وَمَا كَفَرَ سُلَيْمَانُ وَلَٰكِنَّ الشَّيَاطِينَ كَفَرُوا يُعَلِّمُونَ النَّاسَ السِّحْرَ}

[Na wakafuata yale waliyo zua mashet’ani kuuzulia ufalme wa Su leiman. Na wala Suleiman hakukufuru, bali mashet’ani ndio walio kufuru, wakiwafundisha watu uchawi,]

katika aya hii tunaona wazi yakwamba Masheitani wamekufuru kwa sababu wanawafundisha watu uchawi. Na Mtume Muhammad anasema ﷺ:

[اجتنبوا السبع الموبقات]، قالوا: يا رسول الله، وما هن؟ قال: [الشرك بالله، والسحر]   متفق عليه

[Epukeni madhambi saba yenye kuangamiza] Masahaba wakamuliza ni yapi Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ Akasema: [Kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kufanya uchawi]   [Imepokewa na Bukhari na Muslim]

Hivyo basi Muislamu yeyote anaefanya kazi ya uchawi na uganga sio katika sisi na ameshaasi Uislamu na Uislamu uko mbali na yeye, hata ikiwa anaefanya hivyo anajiita Shekhe

Makala haya yameandikwa na

Mahamd Fadhil El Shiraziy

Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.