0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

424. Riyadhu Swalihina Mlango Wa Kutaraji (Rehema Za Mwenyezi Mungu.)

باب الرجاء


وعن أَبي هريرة – رضي الله عنه -، قَالَ: كُنَّا قُعُوداً مَعَ رَسُول الله – صلى الله عليه وسلم -، مَعَنَا أَبُو بَكْرٍ وَعُمْرُ – رضي الله عنهما -، في نَفَرٍ فَقَامَ رَسُول الله – صلى الله عليه وسلم – مِنْ بَيْنِ أظْهُرِنَا، فَأبْطَأَ عَلَيْنَا فَخَشِينَا أنْ يُقتطَعَ دُونَنَا، فَفَزِعْنَا فَقُمْنَا فَكُنْتُ أوَّلَ مَنْ فَزِعَ فَخَرَجْتُ أبْتَغِي رسولَ الله – صلى الله عليه وسلم -، حَتَّى أتَيْتُ حَائِطاً للأنْصَارِ… وَذَكَرَ الحَدِيثَ بِطُولِهِ إِلَى قوله: فَقَالَ رَسُول الله – صلى الله عليه وسلم -: {اذهَبْ فَمَن لَقِيتَ وَرَاءَ هَذَا الحَائِطِ يَشْهَدُ أنْ لا إله إلاَّ الله، مُسْتَيقِناً بِهَا قَلبُهُ فَبَشِّرْهُ بِالجَنَّةِ}      رواه مسلم


شرح الحديث مع فضيلة الشيخ خالد بن عثمان السبت حفظه الله تعالى



Imepokewa kutoka kwa Abû Huraira (Radhi za Allah ziwe juu yake) amesimulia: “Tulikuwa tumeketi pamoja na Mtume , pamoja nasi alikuwepo Abûbakar na ‘Umar (Radhi za Allah ziwe juu yake) katika kundi. Mtume akaondoka miongoni mwetu, akachelewa kurudi kwetu. Tukahofia asije akawa amedhuriwa. Tukafazaika, tukasimama, mimi nilikuwa wa kwanza kufazaika. Nikatoka kwenda kumtafuta Mtume hata nikafika katika bustani moja la Ansari. – akakieleza kisa kwa urefu wake hadi akasema: “Mtume akaniambia: [ Nenda, utakayemkuta nyuma ya bustani hili anashuhudia kuwa hakuna anayestahiki kuabudiwa kwa haki ispokuwa Allâh ilihali ya kuyakinisha kabisa neno hili moyoni mwake, mbashirie Pepo.]   [ Imepokewa na Muslim ]


Begin typing your search above and press return to search.