0%

https://uongofu.com/wp-content/uploads/2021/06/services-head-1.png

18. MLANGO WA KUKATAZA BID’A NA MAMBO YA UZUSHI


BUSTANI YA WATU WEMA


1463655589


{وقال تعالى : {فَمَاذَا بَعْدَ الْحَقِّ إِلَّا الضَّلَالُ

{وقال تعالى : {مَّا فَرَّطْنَا فِي الْكِتَابِ مِن شَيْءٍ

{وقال تعالى : {فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّهِ وَالرَّسُولِ

{وقال تعالى : {وَأَنَّ هَٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ

{وقال تعالى : {قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللَّهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ

والآيات في الباب كثيرة معلومة


Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[Na kipo kitu gani baada ya haki, isipokuwa upotovu tu?]       [Suurat Yunus:32]

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote]       [Suurat An’aam:38]

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume]      [Surat An-Nisaai:59]

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[Na kwa hakika hii ndiyo Njia yangu Iliyo Nyooka. Basi ifuateni, wala msifuate njia nyingine, zikakutengeni na Njia yake.]       [Suurat An’aam:153]

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu]     [Suurat Al ‘Imran:31]

Na Aya katika Mlango huu ni nyingi zenye kujulikana.


شرح مقدمة الباب مع فضيلة الشيخ خالد بن عثمان السبت حفظه الله





Toa maoni yako

Begin typing your search above and press return to search.