{"id":7427,"date":"2021-06-25T13:03:54","date_gmt":"2021-06-25T13:03:54","guid":{"rendered":"https:\/\/uongofu.com\/?p=7427"},"modified":"2022-09-14T08:42:58","modified_gmt":"2022-09-14T08:42:58","slug":"mambo-makubwa-yaliyotokea-kabla-ya-kuzaliwa-mtume","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/uongofu.com\/en\/mambo-makubwa-yaliyotokea-kabla-ya-kuzaliwa-mtume\/","title":{"rendered":"MAMBO MAKUBWA YALIYOTOKEA KABLA YA KUZALIWA MTUME \ufdfa"},"content":{"rendered":"<p style=\"text-align: center;\"><span style=\"font-size: 18pt; color: #0000ff; font-family: terminal, monaco;\">AR-RAHEEQ AL- MAKHTUUM<\/span><\/p>\n<hr \/>\n<p style=\"text-align: left;\">\u00a0<span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Mambo Adhimu Yaliyotokea Kabla Ya Kuja Kwa Muhammad\u00a0<span style=\"color: #008000;\">\ufdfa.<\/span><\/span><br \/>\n<span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Bila shaka jambo lolote adhimu hutanguliwa na matukio, dalili na bishara mbali mbali adhimu yakiwa kama ni ishara ya kulikaribisha jambo hilo. Na wanadamu hawajapata kutokewa na jambo adhimu kuliko hili la kuzaliwa kwa Al-Habiyb Al-Mustwafaa Muhammad\u00a0<\/span><span style=\"color: #008000;\"><span style=\"font-size: 14pt;\">\ufdfa<\/span><span style=\"font-size: 14pt;\">.<\/span><\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: left;\"><span style=\"color: #800000;\"><strong><span style=\"font-size: 14pt;\">KUFUKULIWA KISIMA CHA ZAMZAM\u00a0<\/span><\/strong><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Anasema Ibn Kathiyr katika \u2018Al-Bidaayah wan-Nihaayah\u2019:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cAmesema Ibn Is-haaq; nimehadithiwa na Yaziyd bin Abi Habib Al-Masri kutoka kwa Murthad bin \u2018Abdillaah Al-Yazni kutoka kwa \u2018Abdullaah bin Zarir al-Ghafiqiy kuwa alimsikia \u2018Aliy bin Abi Twaalib (Radhiya Allaahu \u2018anhu) akihadithia hadithi ya Zamzam alipoamrishwa \u2018Abdul-Muttwallib kukichimba. Anasema: \u201cAlisema \u2018Abdul-Muttwallib:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cNilipokuwa nimelala chumbani kwangu nikasikia sauti usingizini ikiniambia: &#8220;Chimba At-Tiyba&#8221;.<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Akasema:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Nikauliza: &#8220;Nini At-Tiyba ?&#8221; lakini mtu huyo akatoweka.<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Ulipoingia usiku wa pili yake nikaenda kitandani pangu kulala na mtu yule akanijia tena usingizini, akaniambia:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Chimba Barrah&#8221; nikamuuliza:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Ni nini hii Barrah?&#8221; kisha akatoweka tena. <\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Na usiku uliofuata nikaenda kitandani pangu kulala, akanijia akaniambia:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Chimba Al-Madhnuwnah,&#8221; nikamuuliza:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Nini Al-Madhnuwnah?\u201d akatoweka. Usiku uliofuata nikaenda kitandani kulala, akanijia tena akaniambia:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Chimba Zamzam&#8221; \u00a0nikamuuliza:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Nini Zamzam?&#8221;<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Akaniambia:<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><span style=\"font-size: 14pt; color: #ff6600;\">\u0644\u0627 \u062a\u0646\u0632\u0641 \u0623\u0628\u062f\u0627\u064b \u0648\u0644\u0627 \u062a\u0630\u0645 \u060c \u062a\u0640\u0633\u0642\u064a \u0627\u0644\u062d\u062c\u064a\u062c \u0627\u0644\u0623\u0639\u0640\u0638\u0645 \u0648\u0647\u064a \u0628\u064a\u0646 \u0627\u0644\u0641\u0631\u062b \u0648\u0627\u0644\u062f\u0645 \u0639\u0646\u062f \u0646\u0642\u0631\u0629 \u0627\u0644\u063a\u0631\u0627\u0628 \u0627\u0644\u0623\u0639\u0635\u0645 \u060c \u0639\u0646\u062f \u0642\u0631\u064a\u0629 \u0627\u0644\u0646\u0645\u0644<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #808000;\"><em><span style=\"font-size: 14pt;\">&#8220;Hakikauki abadan, wala hayapunguwi maji yake. Kitawanywisha mahujaji watukufu,na kipo baina ya mavi na damu, karibu na mahali atakapodokowa kunguru mwenye miguu meusi, penye kichungu cha sisimizi.&#8221;<\/span><\/em><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Anasema Ibn Is-haaq:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Alipojulisha utukufu wake na kufahamishwa mahali kilipo na alipojua kuwa aliyoyasikia ni ya kweli, asubuhi ilipoiniga akachukua jembe lake na kuondoka pamoja na mwanawe Al-Haarith, na wakati huo hakuwa na mtoto mwengine isipokuwa huyo, akaanza kuchimba na alipoyafikia maji akapiga takbir, na Maquraysh watu wa kabila la Bani Umayyah wanaotokana na Bani Abdu Manaf wakajua kuwa keshapata alichokitaka wakamwendea na kumwambia:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cEwe \u2018Abdul-Muttwallib! Hiki ni kisima cha baba yetu Ismaail, na sisi tuna haki yetu ndani yake kwa hivyo utushirikishe na sisi pia.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Akasema:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Sitofanya hivyo, jambo hili nimehusishwa nalo peke yangu na nyinyi hamumo na nimechaguliwa mimi kati yenu nyote.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Wakamwambia:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Tupe haki yetu kwani sisi hatutokuacha mpaka tumtafute atakayehukumu baina yetu.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Akasema:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Mchagueni mnayemtaka ahukumu baina yetu.&#8221;<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Wakasema:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cMpiga ramli mwanamke wa kabila la Bani Sa\u2019ad Hudhaym.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Akasema:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cNimekubali.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Anasema Ibnu Is-haaq:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cMpiga ramli huyo alikuwa akiishi karibu na nchi ya Shaam, na \u2018Abdul-Muttwallib akapanda farasi wake, nao wakapanda farasi wao pia, na kutoka katika kila kabila akatoka mtu mmoja, wakafuatana na kuianza safari ndefu kuelekea Sham., na ardhi yote wakati huo ilikuwa jangwa, walipofika katika sehemu mojawapo ya jangwa hilo iliyopo baina ya Hijjahz na Sham maji ya \u2018Abdul-Muttwallib na ya wenzake yakamalizika, wakashikwa na kiu na walipotambua kuwa watakuja kufa kiu, wakawaomba Maquraysh waliofuatana nao, wakakataa wakasema:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cNa sisi tuko jangwani pia, tunajiogopea nafsi zetu yasije yakatukuta yalokukuteni.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u2018Abdul-Muttwallib akawauliza wenzake:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cMnaonaje?\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Wakasema:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cTupe rai yako na sisi tuko tayari kukufuata.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Akasema:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cMimi naona kwa vile bado tuna nguvu zetu, bora kila mmoja wenu ajichimbie shimo lake na kila atakapokufa mmoja, basi wenzake wamsukume ndani ya shimo lake kisha wamfukie mpaka atakapobaki mmoja tu kati yenu, na akipotea mtu mmoja bora kuliko kupotea kundi zima.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Wakasema:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cRai yako ni nzuri sana.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Wakashuka, na kila mmoja wao akaanza kujichimbia shimo lake kisha wakakaa kila mmoja akisubiri kifo chake.<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u2018Abdul-Muttwallib akawaambia wenzake\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">\u201cWaLlaahi huku kukaa kwetu tukiyangoja mauti ni uvivu, kwa nini tusiendelee na safari, huenda tukabahatika kuufikia mji tukapata maji? Inukeni tuendelee na safari.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Wakainuka na kumsubiri \u2018Abdul-Muttwallib apande farasi wake, na alipokuwa akimpanda farasi wake, pakatokea mpasuko chini ya farasi wake na maji matamu yakaanza kutoka, akawaita makabila yote ya Kiquraysh aliofuatana nao akawaambia:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;Njooni mpate kunywa maji, kwani Allaah ndiye aliyetuletea maji haya, kwa hivyo kunyweni, jazeni viriba vyenu na wapeni farasi wenu pia.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Wenzake wakasema:<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">&#8220;WaLlaahi Allaah keshatoa uamuzi wake juu ya kisima cha maji ya Zamzam, kwa hivyo hatutoshindana na wewe abadan. Bali yule aliyekuletea maji katika jangwa hili ndiye aliyekuletea kisima cha Zamzam, kwa hivyo rudi katika kisima chako ukiwa mshindi.&#8221;<\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size: 14pt; color: #000000;\">Wakarudi wote pamoja na hawakumuendea tena mpiga ramli.<span style=\"font-size: 12pt;\">[1]<\/span><\/span><\/p>\n<hr \/>\n<p><span style=\"font-size: 12pt;\">[1]\u00a0<span style=\"font-size: 16px; color: #000000;\">Muhammad \ufdfa Rahma Kwa Walimwengu.<\/span><\/span><\/p>\n<hr \/>","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>AR-RAHEEQ AL- MAKHTUUM \u00a0Mambo Adhimu Yaliyotokea Kabla Ya Kuja Kwa Muhammad\u00a0\ufdfa. Bila shaka jambo lolote adhimu hutanguliwa na matukio, dalili na bishara mbali mbali adhimu yakiwa kama ni ishara ya kulikaribisha jambo hilo. Na wanadamu hawajapata kutokewa na jambo adhimu kuliko hili la kuzaliwa kwa Al-Habiyb Al-Mustwafaa Muhammad\u00a0\ufdfa. KUFUKULIWA KISIMA CHA ZAMZAM\u00a0 Anasema Ibn Kathiyr [&hellip;]<\/p>","protected":false},"author":2,"featured_media":15476,"comment_status":"open","ping_status":"closed","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"_acf_changed":false,"give_campaign_id":0,"_bbp_topic_count":0,"_bbp_reply_count":0,"_bbp_total_topic_count":0,"_bbp_total_reply_count":0,"_bbp_voice_count":0,"_bbp_anonymous_reply_count":0,"_bbp_topic_count_hidden":0,"_bbp_reply_count_hidden":0,"_bbp_forum_subforum_count":0,"footnotes":""},"categories":[57],"tags":[],"class_list":["post-7427","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","hentry","category-sera-ya-mtume"],"acf":[],"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/7427","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/users\/2"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/comments?post=7427"}],"version-history":[{"count":8,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/7427\/revisions"}],"predecessor-version":[{"id":15489,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/7427\/revisions\/15489"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/media\/15476"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/media?parent=7427"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/categories?post=7427"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/tags?post=7427"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}