{"id":4841,"date":"2021-06-17T21:24:01","date_gmt":"2021-06-17T21:24:01","guid":{"rendered":"https:\/\/uongofu.com\/?p=4841"},"modified":"2023-05-10T08:20:57","modified_gmt":"2023-05-10T08:20:57","slug":"maisha-yake-wakati-wa-mtume-%ef%b7%ba","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/uongofu.com\/en\/maisha-yake-wakati-wa-mtume-%ef%b7%ba\/","title":{"rendered":"MAISHA YAKE WAKATI WA MTUME \ufdfa"},"content":{"rendered":"<h4><span style=\"color: #993300;\">MAISHA YAKE WAKATI WA MTUME \ufdfa<\/span><\/h4>\n<p>&#8216;Uthman alikuwa miongoni mwa marafiki wa Abu Bakar (r.a.).\u00a0Walikuwa katika kikao siku moja, akawa Abu Bakar (r.a.)\u00a0anamfafanulia uzuri wa Uislamu, na ubaya wa shirki. Alikuwa\u00a0&#8216;Uthman (r.a.) si mwenye kutaradadi, akaathirika na maneno ya Abu\u00a0Bakar (r.a.) kisha wakaenda pamoja kwa Mtume \ufdfa,\u00a0walipokutana na Mtume \ufdfa alimlingania kwa Uislamu\u00a0akasilimu.<\/p>\n<p>Akawa miongoni mwa watu waliotangulia katika Uislamu.Wakaathirika vibaya Maquraysh kwa kusilimu &#8216;Uthman (r.a.). Ami\u00a0yake\u00a0Al-Hakam ibn Abil &#8216;Aas\u00a0alifanya kila bidii ya kumtoa &#8216;Uthman\u00a0(r.a.) katika kundi la walslamu, lakini hakufanikiwa, kisha\u00a0akamuadhibu adhabu kali, lakini &#8216;Uthman (r.a.) akavumilia adhabu\u00a0hizo na akawa ni mwenye msimamo. Pia mama yake alijaribu\u00a0kutaka kumtoa &#8216;Uthman katika Uislamu, lakini hakuweza.<\/p>\n<p>Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0alimuoza binti yake ambaye ni Ruqayyah. Maudhi ya\u00a0Maquraish yalipozidi juu ya &#8216;Uthman (r.a.) aliamua kuhama na\u00a0mkewe katika mwezi wa Mfungo Kumi, mwaka wa Tano wa Utume\u00a0mpaka Habasha nchi ya Ethiopia. Kisha wakarudi Makkah na mkewe\u00a0Mfungo Mosi mwaka huo huo. Kisha &#8216;Uthman (r.a.) akahamia\u00a0Madinah baada ya kuhamia huko Mtume\u00a0\ufdfa, Kwa sababu hiyo\u00a0akaitwa &#8220;Mwenye kuhamia mara mbili.<\/p>\n<p>Mtume \ufdfa alipoenda katika vita vya Badri, alimbakisha &#8216;Uthman (r.a.) Madinah ili kumuuguza mkewe. Akafariki mkewe kabla ya Mtume \ufdfa kurudi kutoka vita vya Badri. &#8216;Uthman (r.a.) akahuzunika sana kwa kufariki mkewe. Na kwa nini asihuzunike ili hali umekatika ukwe kati yake na Mtume \ufdfa\u00a0\u00a0Mtume \ufdfa akamtuliza moyo &#8216;Uthman kwa kumuoza binti yake mwengine, Ummu-Kulthum (r.a.). Akaishi naye &#8216;Uthman mpaka alipofariki mwaka wa Tisa wa Hijrah.<\/p>\n<p>Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0akamwambia\u00a0&#8216;Uthrnan:<\/p>\n<p dir=\"rtl\" style=\"text-align: center;\"><span style=\"color: #008000;\">[\u0648\u0627\u0644\u0630\u064a \u0646\u0641\u0633\u064a \u0628\u064a\u062f\u0647 \u0644\u0648 \u0643\u0627\u0646 \u0639\u0646\u062f\u064a \u062b\u0627\u0644\u062b\u0629 \u0644\u0632\u0648\u064e\u0651\u062c\u062a\u064f\u0643\u064e\u0647\u0627 \u064a\u0627 \u0639\u062b\u0645\u0627\u0646]<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\">[Naapa kwa yule nafsi yangu iko mikononi mwake Lau kama ningekua na binti wa tatu ningekuozesha Ewe Uthma.]<\/span><\/p>\n<p>Kwa\u00a0sababu &#8216;Uthman alioa mabinti wawili wa Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0ndipo\u00a0akaitwa\u00a0&#8220;Dhan-Nurain&#8221;\u00a0(mwenye nuru mbili).<\/p>\n<p>Alikuwa &#8216;Uthman ana mali mengi kuliko Masahaba wote. Kwa sababu\u00a0hiyo alitoa mali zaidi ya wote kwa vita vya Tabuk. Ukafikia mchango\u00a0wake ngamia mia tisa, na farasi khamsini. Na alipokuja na Dinari\u00a0elfu moja za dhahabu akaziweka mbele ya Mtume (s.a.w.) ambaye<br \/>\nakawa anazigeuza huku na huku kwa mikono yake, akisema:<\/p>\n<p dir=\"rtl\" style=\"text-align: center;\"><span style=\"color: #008000;\">[\u0645\u0627 \u0636\u0631 \u0639\u062b\u0645\u0627\u0646 \u0645\u0627 \u0639\u0645\u0644 \u0628\u0639\u062f \u0647\u0630\u0627 \u0627\u0644\u064a\u0648\u0645]<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\">[Hatadhurika &#8216;Uthrnan na atakalofanya baada ya lea.]<\/span><\/p>\n<p>Kwa sababu\u00a0hiyo aliitwa &#8220;Muandalizi wa jeshi liliokuwa na uzito.&#8221;\u00a0&#8216;Uthman (r.a.) alinunua kisima cha Rumah kwa Dirham 20,000\u00a0kutoka kwa Myahudi mmoja, kisha akakifanya waqfu. Na ilikuwa\u00a0hakuna maji matamu ya kunywa Madinah isipokuwa kwenye kisima\u00a0hicho. Kisha ikawa nasibu yake ni kuteka maji kama WaIslamu\u00a0wengine.<\/p>\n<p>Pia &#8216;Uthrnan (r.a.) alishiriki katika vita vyote pamoja na Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0isipokuwa vita vya Badri kama tulivyotangulia kueleza. Na\u00a0pia alikuwa &#8216;Uthman (r.a.) ndiye mjumbe wa Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0kwa\u00a0Maquraysh katika Sulhu ya AI-Hudaybiyyah. Alipokwenda Makkah\u00a0kwa amri ya Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0akachelewa kurudi, ukaenea uvumi\u00a0kuwa &#8216;Uthrnan (r.a.) arneuawa, walienda WaIslamu kwa Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0ambaye alikuwa chini ya mti wakambayi&#8217; juu ya kupigana\u00a0na Maquraysh, na wakachukua ahadi kuwa hawatakimbia wakati wa\u00a0vita. Kisha Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0akachukua mkono wake, na akasema:<\/p>\n<p dir=\"rtl\" style=\"text-align: center;\"><span style=\"color: #008000;\">[\u0647\u0630\u0647 \u064a\u062f \u0639\u062b\u0645\u0627\u0646]<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\">[Huu ni mkono wa &#8216;Uthman]\u00a0<span style=\"color: #000000;\">akaupiga juu ya mkono wake wa\u00a0kushoto, na akasema: &#8220;Na hii ni bay&#8217;ah ya &#8216;Uthrnan.&#8221; Ikawa ni\u00a0Bay&#8217;ah ya Ar-Ridhwan. Na kwa juu ya hayo limeashiria<\/span><\/span><br \/>\nNeno lake\u00a0Allah Aliyetukuka Allposema:<\/p>\n<p dir=\"rtl\" style=\"text-align: center;\"><span style=\"color: #008000;\">{\u0644\u0651\u064e\u0642\u064e\u062f\u0652 \u0631\u064e\u0636\u0650\u064a\u064e \u0627\u0644\u0644\u0651\u064e\u0647\u064f \u0639\u064e\u0646\u0650 \u0627\u0644\u0652\u0645\u064f\u0624\u0652\u0645\u0650\u0646\u0650\u064a\u0646\u064e \u0625\u0650\u0630\u0652 \u064a\u064f\u0628\u064e\u0627\u064a\u0650\u0639\u064f\u0648\u0646\u064e\u0643\u064e \u062a\u064e\u062d\u0652\u062a\u064e \u0627\u0644\u0634\u0651\u064e\u062c\u064e\u0631\u064e\u0629\u0650 \u0641\u064e\u0639\u064e\u0644\u0650\u0645\u064e \u0645\u064e\u0627 \u0641\u0650\u064a \u0642\u064f\u0644\u064f\u0648\u0628\u0650\u0647\u0650\u0645\u0652 \u0641\u064e\u0623\u064e\u0646\u0632\u064e\u0644\u064e \u0627\u0644\u0633\u0651\u064e\u0643\u0650\u064a\u0646\u064e\u0629\u064e \u0639\u064e\u0644\u064e\u064a\u0652\u0647\u0650\u0645\u0652 \u0648\u064e\u0623\u064e\u062b\u064e\u0627\u0628\u064e\u0647\u064f\u0645\u0652 \u0641\u064e\u062a\u0652\u062d\u064b\u0627 \u0642\u064e\u0631\u0650\u064a\u0628\u064b\u0627}<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><em>[Kwa hakika Mwenyezi Mungu amewapa radhi Waumini walipo fungamana nawe chini ya mti, na alijua yaliyomo nyoyoni mwao. Basi akateremsha utulivu juu yao, na akawalipa kwa Ushindi wa karibu.]<\/em><\/span><\/p>\n<blockquote><p>\u00a0<em>Al Khulafaau Arrashiduun 103-105<\/em><\/p><\/blockquote>","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>MAISHA YAKE WAKATI WA MTUME \ufdfa &#8216;Uthman alikuwa miongoni mwa marafiki wa Abu Bakar (r.a.).\u00a0Walikuwa katika kikao siku moja, akawa Abu Bakar (r.a.)\u00a0anamfafanulia uzuri wa Uislamu, na ubaya wa shirki. Alikuwa\u00a0&#8216;Uthman (r.a.) si mwenye kutaradadi, akaathirika na maneno ya Abu\u00a0Bakar (r.a.) kisha wakaenda pamoja kwa Mtume \ufdfa,\u00a0walipokutana na Mtume \ufdfa alimlingania kwa Uislamu\u00a0akasilimu. Akawa miongoni [&hellip;]<\/p>","protected":false},"author":2,"featured_media":20185,"comment_status":"open","ping_status":"closed","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"_acf_changed":false,"give_campaign_id":0,"_bbp_topic_count":0,"_bbp_reply_count":0,"_bbp_total_topic_count":0,"_bbp_total_reply_count":0,"_bbp_voice_count":0,"_bbp_anonymous_reply_count":0,"_bbp_topic_count_hidden":0,"_bbp_reply_count_hidden":0,"_bbp_forum_subforum_count":0,"footnotes":""},"categories":[63],"tags":[],"class_list":["post-4841","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","hentry","category-uthman-ibn-affan"],"acf":[],"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/4841","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/users\/2"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/comments?post=4841"}],"version-history":[{"count":5,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/4841\/revisions"}],"predecessor-version":[{"id":20187,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/4841\/revisions\/20187"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/media\/20185"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/media?parent=4841"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/categories?post=4841"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/tags?post=4841"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}