{"id":4672,"date":"2021-06-17T08:38:19","date_gmt":"2021-06-17T08:38:19","guid":{"rendered":"https:\/\/uongofu.com\/?p=4672"},"modified":"2022-10-17T12:30:31","modified_gmt":"2022-10-17T12:30:31","slug":"kuwatendea-wema-wazazi-wawili","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/uongofu.com\/en\/kuwatendea-wema-wazazi-wawili\/","title":{"rendered":"KUWATENDEA WEMA WAZAZI WAWILI"},"content":{"rendered":"<h3><span style=\"color: #993300;\">KUWATENDEA\u00a0WEMA WAZAZI WAWILI<\/span><\/h3>\n<p>Wazazi wawili wanayo haki kubwa kutoka kwa watoto wao, kama walivyo na haki watoto kutoka kwa wazazi wao. Mwenyezi Mungu\u00a0<span style=\"color: #008080;\">\ufdfb<\/span>\u00a0Ameweka wazi kabisa haki za Pande zote mbili. Mwenyezi Mungu hakuwaachia wanadamu wajipangie wenyewe haki zao, bali Yeye Mwenyewe Amechukua jukumu la kuwapangia kila moja haki yake ili asipatikane na upungufu au dhulma katika kugawa hizo haki. Wazazi wana nafasi kubwa katika Dini ya Kiislamu. Wao ndio sababu ya kupatikana mtoto, baada ya kuvumilia na kusubiri juu ya shida nyingi kisha kuzaliwa mtoto. Kwa kuvumilia kwao na kusubiri juu ya shida zote, wamepata cheo kikubwa mbele ya Mwenyezi Mungu\u00a0<span style=\"color: #008080;\">\ufdfb<\/span>.<\/p>\n<p>Mwenyezi Mungu\u00a0\ufdfb\u00a0ameambatanisha haki yake pamoja na haki ya wazazi wa wili. katika aya kadha katika kitabu chake kitukufu, nayo ni haki ya wazazi wawili. Jueni kwamba mafungamano makubwa baina ya mja na Mola wake ni kuumcha Mwenyezi Mungu\u00a0<span style=\"color: #008080;\">\ufdfb<\/span>\u00a0na kusimamia haki za wazazi na kusimamia haki za waja wake.<\/p>\n<p>Amesema Mwenyezi Mungu\u00a0\u00a0\ufdfb<\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><span style=\"color: #008000;\">\u0648\u064e\u0627\u0639\u0652\u0628\u064f\u062f\u064f\u0648\u0627 \u0627\u0644\u0644\u0651\u064e\u0647\u064e \u0648\u064e\u0644\u064e\u0627 \u062a\u064f\u0634\u0652\u0631\u0650\u0643\u064f\u0648\u0627 \u0628\u0650\u0647\u0650 \u0634\u064e\u064a\u0652\u0626\u064b\u0627 \u06d6 \u0648\u064e\u0628\u0650\u0627\u0644\u0652\u0648\u064e\u0627\u0644\u0650\u062f\u064e\u064a\u0652\u0646\u0650 \u0625\u0650\u062d\u0652\u0633\u064e\u0627\u0646\u064b\u0627} \u0627\u0644\u0646\u0633\u0627\u0621 :36}<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><em>[Mwabuduni Mwenyezi Mungu wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni wema wazazi wawili]<\/em>\u00a0 \u00a0 \u00a0[Al Nnissa:36]<\/span><\/p>\n<p>Jueni waja wa Mwenyezi Mungu kwamba kuwafanyia wema wazazi wawili ni wajibu hata kama ni makafiri, imepokewa na Asema:<\/p>\n<p style=\"text-align: right;\"><span style=\"color: #008000;\">\u0642\u062f\u0645\u062a\u0652 \u0639\u0644\u064a\u0651 \u0623\u0645\u064a \u0648\u0647\u064a \u0645\u0634\u0631\u0643\u0629 \u0641\u064a \u0639\u0647\u062f \u0631\u0633\u0648\u0644 \u0627\u0644\u0644\u0647 -\u0635\u0644\u0649 \u0627\u0644\u0644\u0647 \u0639\u0644\u064a\u0647 \u0648\u0633\u0644\u0645-\u060c \u0641\u0627\u0633\u062a\u0641\u062a\u064a\u062a \u0631\u0633\u0648\u0644 \u0627\u0644\u0644\u0647 -\u0635\u0644\u0649 \u0627\u0644\u0644\u0647 \u0639\u0644\u064a\u0647 \u0648\u0633\u0644\u0645-\u060c \u0642\u0644\u062a: \u0648\u0647\u064a \u0631\u0627\u063a\u0628\u0629\u060c \u0623\u0641\u0623\u0635\u0644 \u0623\u0645\u064a\u061f \u0642\u0627\u0644: \u0646\u0639\u0645\u060c \u0635\u0644\u064a \u0623\u0645\u0643 \u0631\u0648\u0627\u0647 \u0627\u0644\u0628\u062e\u0627\u0631\u064a \u0648\u0645\u0633\u0644\u0645<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\">[Amenijia mamangu na yeye ni mshirikina wakati wa Ahadi ya mtume (yani kipindi mtume amefanya itafaki a mushrikina ) nikamuliza Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0ni kasema (amenija) na yeye ataka ni muunge je ni muunge mamangu? Akasema Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0: [Ndio muunge mamako].\u00a0[Imepokewa na Bukhari na Muslim].<\/span><\/p>\n<p>Wema kwa wazazi haukatiki hata kama watakuamrisha kumkufuru Mwenyezi Mungu na kumshirikisha.Isipokuwa itakuwa haifai kuwatii kwa hilo.<\/p>\n<p>Amesema Mwenyezi Mungu\u00a0<span style=\"color: #008080;\">\ufdfb<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: right;\"><span style=\"color: #008000;\">\u0648\u064e\u0648\u064e\u0635\u0651\u064e\u064a\u0652\u0646\u064e\u0627 \u0627\u0644\u0652\u0625\u0650\u0646\u0633\u064e\u0627\u0646\u064e \u0628\u0650\u0648\u064e\u0627\u0644\u0650\u062f\u064e\u064a\u0652\u0647\u0650 \u062d\u064e\u0645\u064e\u0644\u064e\u062a\u0652\u0647\u064f \u0623\u064f\u0645\u0651\u064f\u0647\u064f \u0648\u064e\u0647\u0652\u0646\u064b\u0627 \u0639\u064e\u0644\u064e\u0649\u0670 \u0648\u064e\u0647\u0652\u0646\u064d \u0648\u064e\u0641\u0650\u0635\u064e\u0627\u0644\u064f\u0647\u064f \u0641\u0650\u064a \u0639\u064e\u0627\u0645\u064e\u064a\u0652\u0646\u0650 \u0623\u064e\u0646\u0650 \u0627\u0634\u0652\u0643\u064f\u0631\u0652 \u0644\u0650\u064a \u0648\u064e\u0644\u0650\u0648\u064e\u0627\u0644\u0650\u062f\u064e\u064a\u0652\u0643\u064e \u0625\u0650\u0644\u064e\u064a\u0651\u064e \u0627\u0644\u0652\u0645\u064e\u0635\u0650\u064a\u0631\u064f\u0648\u064e\u0625\u0650\u0646 \u062c\u064e\u0627\u0647\u064e\u062f\u064e\u0627\u0643\u064e \u0639\u064e\u0644\u064e\u0649\u0670 \u0623\u064e\u0646 \u062a\u064f\u0634\u0652\u0631\u0650\u0643\u064e \u0628\u0650\u064a \u0645\u064e\u0627 \u0644\u064e\u064a\u0652\u0633\u064e \u0644\u064e\u0643\u064e \u0628\u0650\u0647\u0650 \u0639\u0650\u0644\u0652\u0645\u064c \u0641\u064e\u0644\u064e\u0627 \u062a\u064f\u0637\u0650\u0639\u0652\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u06d6 \u0648\u064e\u0635\u064e\u0627\u062d\u0650\u0628\u0652\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0641\u0650\u064a \u0627\u0644\u062f\u0651\u064f\u0646\u0652\u064a\u064e\u0627 \u0645\u064e\u0639\u0652\u0631\u064f\u0648\u0641\u064b\u0627 \u06d6 \u0648\u064e\u0627\u062a\u0651\u064e\u0628\u0650\u0639\u0652 \u0633\u064e\u0628\u0650\u064a\u0644\u064e \u0645\u064e\u0646\u0652 \u0623\u064e\u0646\u064e\u0627\u0628\u064e \u0625\u0650\u0644\u064e\u064a\u0651\u064e \u06da \u062b\u064f\u0645\u0651\u064e \u0625\u0650\u0644\u064e\u064a\u0651\u064e \u0645\u064e\u0631\u0652\u062c\u0650\u0639\u064f\u0643\u064f\u0645\u0652 \u0641\u064e\u0623\u064f\u0646\u064e\u0628\u0651\u0650\u0626\u064f\u0643\u064f\u0645 \u0628\u0650\u0645\u064e\u0627 \u0643\u064f\u0646\u062a\u064f\u0645\u0652 \u062a\u064e\u0639\u0652\u0645\u064e\u0644\u064f\u0648\u0646} \u0644\u0642\u0645\u0627\u0646:14-15<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><em>[Na tumemuusia mwanadamu kuwafanyia ihsani wazazi wake mama yake ameichukua mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu, na kumnyonyesha na kuja kumuachisha kunyonya katika miaka miwili- basi unishukuru Mimi na wazazi wako; marejeo yenu ni kwangu. Na wazazi wako wakikushurutisha kunishirikisha na yale ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani]<\/em>\u00a0 \u00a0[Luqman:14-15]<\/span><\/p>\n<p>Na Mtume wa Mwenyezi Mungu alitanguliza haki za wazazi wawili kuliko jihadi. Imepokewa Hadithi na \u2018Abdillah Ibn Mas\u2019oud Amesema:<\/p>\n<p style=\"text-align: right;\"><span style=\"color: #008000;\">\u0633\u0623\u0644\u062a \u0627\u0644\u0646\u0628\u064a -\u0635\u0644\u0649 \u0627\u0644\u0644\u0647 \u0639\u0644\u064a\u0647 \u0648\u0633\u0644\u0645- \u0623\u064a \u0627\u0644\u0639\u0645\u0644 \u0623\u062d\u0628 \u0625\u0644\u0649 \u0627\u0644\u0644\u0647 \u062a\u0639\u0627\u0644\u0649\u061f \u0642\u0627\u0644: \u0627\u0644\u0635\u0644\u0627\u0629 \u0639\u0644\u0649 \u0648\u0642\u062a\u0647\u0627\u060c \u0648\u0642\u0627\u0644: \u0642\u0644\u062a: \u062b\u0645 \u0623\u064a\u061f \u0642\u0627\u0644: \u0628\u0631 \u0627\u0644\u0648\u0627\u0644\u062f\u064a\u0646\u060c \u0642\u0644\u062a: \u062b\u0645 \u0623\u064a\u061f \u0642\u0627\u0644: \u0627\u0644\u062c\u0647\u0627\u062f \u0641\u064a \u0633\u0628\u064a\u0644 \u0627\u0644\u0644\u0647 \u0645\u062a\u0641\u0642 \u0639\u0644\u064a\u0647<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\">[Nimemuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu ni amali gani inayo pendeza mbele ya Mwenyezi Mungu? Akasema: Kuswali kwa wakati wake. Nikasema kisha ni amali gani? Akasema: kuwafanyia wema wazazi wawili. Nikasema kisha amali gani? Akasema: jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu.]\u00a0 \u00a0\u00a0[Imepokewa na Bukhari na Muslim]<\/span><\/p>\n<p>Imepokewa na\u00a0Muawiya bin Jahim\u00a0Amesema: Amekuja mtu kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu akasema nataka kwenda jihadi, na nimekuja kukushauri. Akasema Mtume \ufdfa je una mama? Akasema ndio. Akasema Mtume\u00a0<span style=\"color: #008000;\">\ufdfa<\/span>\u00a0jilazimishe na mama yako, kwani pepo iko chini ya miguu yake.<\/p>\n<p>Na Mtume\u00a0<span style=\"color: #008000;\">\ufdfa<\/span>\u00a0anaomba kwa aliyepata wazazi wawili au mmoja wao na hakuingia peponi kwasababu yao basi mtu huyu amekhasirika].<\/p>\n<p>Na visa vya wale watu watatu waliofunikwa na pango na hawakuweza kutoka akasema mmoja wao angalieni amali njema mliyomfanyia Mwenyezi Mungu, mumuombe Mwenyezi Mungu kupitia amali hiyo huenda Mwenyezi Mungu akatufariji, akasema mmoja wao: nilikuwa na wazazi wawili watu wazima na nilikuwa na watoto wadogo na nilikuwa nikiwachungia na ninapokamua nawanywesha wazazi wangu kabla ya watoto wangu, nilipokuja jioni na maziwa nimewakuta wamelala, nikaona vibaya kuwaamsha, pia nikachukia kumtanguliza mtoto wangu kabla yao na mtoto wangu alikuwa akilia na ilikuwa hivyo mpaka alfajiri, ewe Mwenyezi Mungu ukijua tendo langu hilo nikutaka radhi zako\u00a0basi tufariji, Mwenyezi Mungu akawafariji mpaka wakawa wanaona mbingu.<\/p>\n<p>Na katika kuwatendea wema ni kuwatii maadamu hujakhalifu amri ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, Amesema Mwenyezi Mungu\u00a0\ufdfb:<\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><span style=\"color: #008000;\">{\u0648\u064e\u0635\u064e\u0627\u062d\u0650\u0628\u0652\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0641\u0650\u064a \u0627\u0644\u062f\u0651\u064f\u0646\u0652\u064a\u064e\u0627 \u0645\u064e\u0639\u0652\u0631\u064f\u0648\u0641\u064b\u0627}<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><em>[Kaa na wao kwa wema hapa duniani&#8221;]<\/em><\/span><\/p>\n<p>Na haki yao ni kuwapatia matumizi na kuwavisha ikiwa ni maskini, na kuwaombea Mwenyezi Mungu wakiwa hai na baada ya kufa Amesema Mwenyezi Mungu\u00a0<span style=\"color: #008080;\">\ufdfb<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: right;\"><span style=\"color: #008000;\">\u0648\u064e\u0642\u064e\u0636\u064e\u0649\u0670 \u0631\u064e\u0628\u0651\u064f\u0643\u064e \u0623\u064e\u0644\u0651\u064e\u0627 \u062a\u064e\u0639\u0652\u0628\u064f\u062f\u064f\u0648\u0627 \u0625\u0650\u0644\u0651\u064e\u0627 \u0625\u0650\u064a\u0651\u064e\u0627\u0647\u064f \u0648\u064e\u0628\u0650\u0627\u0644\u0652\u0648\u064e\u0627\u0644\u0650\u062f\u064e\u064a\u0652\u0646\u0650 \u0625\u0650\u062d\u0652\u0633\u064e\u0627\u0646\u064b\u0627 \u06da \u0625\u0650\u0645\u0651\u064e\u0627 \u064a\u064e\u0628\u0652\u0644\u064f\u063a\u064e\u0646\u0651\u064e \u0639\u0650\u0646\u062f\u064e\u0643\u064e \u0627\u0644\u0652\u0643\u0650\u0628\u064e\u0631\u064e \u0623\u064e\u062d\u064e\u062f\u064f\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0623\u064e\u0648\u0652 \u0643\u0650\u0644\u064e\u0627\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0641\u064e\u0644\u064e\u0627 \u062a\u064e\u0642\u064f\u0644 \u0644\u0651\u064e\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0623\u064f\u0641\u0651\u064d \u0648\u064e\u0644\u064e\u0627 \u062a\u064e\u0646\u0652\u0647\u064e\u0631\u0652\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0648\u064e\u0642\u064f\u0644 \u0644\u0651\u064e\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0642\u064e\u0648\u0652\u0644\u064b\u0627 \u0643\u064e\u0631\u0650\u064a\u0645\u064b\u0627<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><em>[Na Mola wako amehukumu kuwa msimuabudu yoyote ila Yeye tu. Na kuwafanyia wema wazazi. Kama mmoja wao akifikia uzee, naye yuko pamoja nawe, au wote wawili, basi usiwaambie hata Ah. Wala usiwakemee. Na useme nao kwa msemo wa heshima&#8221;]<\/em><\/span><\/p>\n<p>Imepokewa na Ibn \u2018Umar kwamba yeye akitoka kuelekea Makkah alikuwa na punda na kilemba amejifunga nacho kichwani, siku moja alikutana na Bedui, akasema Bedui yule kumwambia Ibn \u2018Umar Je, wewe si mtoto wa fulani? Ibn \u2018Umar akasema ndio. Pale pale Ibn \u2018Umar akampa punda yule Bedui ampande na kilemba ajifunge. Baadhi ya Maswahaba wakasema Mwenyezi Mungu akusamehe umempatia bedui huyu punda ambaye kwamba ulikuwa ukitembea naye na kilemba uliyokuwa umejifunga nacho. Akasema amesema Mtume \ufdfa [Bora ya wema ni kuunga mtu vipenzi vya babake baada ya kuondoka duniani].<\/p>\n<p><span style=\"color: #993300;\">THAWABU ZA KUWATENDEA WEMA WAZAZI WAWILI<\/span><\/p>\n<p>Kuwatendea wema wazazi wawili ni sababu ya kuingia peponi, je umepata kujua kisa cha\u00a0Uweis Bin Annur Al-Qarni?\u00a0Huyu ni mtu aliyesimuliwa na Mtume kisa chake na akaamrisha maswahaba zake kutaka dua kutoka kwake, na kukurubishwa kwa Mwenyezi Mungu na haikuwa alama yake isipokuwa kuponya, hadithi ambayo ameipokea Imam Muslim inaeleza kuwa \u2018Umar alijiwa na pote kutoka Yemen akauliza jee kuna Uweis kati yenu? Mpaka alipokuja Uweis akasema wewe ndio Uwes? Akasema \u2018Umar jee ulikuwa na ugonjwa wa ukoma ukapona isipokuwa sehemu kama ya shilingi, akasema ndio, akasema \u2018Umar jee una mama? Akasema ndiyo. Akasema nimemsikia Mtume\u00a0\ufdfa\u00a0akisema:\u00a0[Atakujieni Uweis na pote kutoka Yemen na alikuwa na ukoma na akapona ila sehemu ya shilingi na alikuwa mwema kwa mamake akimuapia Mwenyezi Mungu huwa jambo hilo ukiweza akuombee msamaha]\u00a0Akasema \u2018Umar niombee msamaha na akamuombea \u2018Umar msamaha.<\/p>\n<p>Na Muhammad\u00a0Ibn Sirin\u00a0alikuwa akinyenyekea anapozungumza na mamake.<\/p>\n<p>Hassan bin \u2018Ali Ibn Hussein Zeinul \u2018Abidin alikuwa akimfanyia wema mamake mpaka akaulizwa siku moja, kwa nini hatukuoni ukila sahani moja na mamako? Akasema naogopa kutangulia mkono wangu sehemu ambao kwamba jicho la mama limekwisha kutangulia, na hapo nitakuwa nimemuasi.<\/p>\n<p>Na huyu\u00a0Shureyh\u00a0alikuwa ni miongoni mwa wanazuoni wakubwa alikuwa akiwafundisha wanafunzi wanaokuja kutoka sehemu mbali mbali na mamake alikuwa akimtuma kwa kumwambia awapatie chakula kuku, basi husimama na kuacha kufundisha. Huu ni mfano wa watu wema waliotangulia, vipi hali ya barobaro wetu leo huenda mmoja wao kukosea heshima mzazi wake na kumridhisha rafiki yake. Nakuusieni kuwafanyia wema wazazi wenu na kwenda mbio kuwaridhisha wao.<\/p>\n<hr \/>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>SIKILIZA MADA HII NA SHEIKH SWADIQ ALI<\/em><\/p>\n<hr \/>\n<p><audio style=\"display: block; margin: 9px auto;\" src=\"https:\/\/archive.org\/download\/KuwatendaWema\/kuwatenda%20wema.mp3\" controls=\"controls\"><\/audio><\/p>","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>KUWATENDEA\u00a0WEMA WAZAZI WAWILI Wazazi wawili wanayo haki kubwa kutoka kwa watoto wao, kama walivyo na haki watoto kutoka kwa wazazi wao. Mwenyezi Mungu\u00a0\ufdfb\u00a0Ameweka wazi kabisa haki za Pande zote mbili. Mwenyezi Mungu hakuwaachia wanadamu wajipangie wenyewe haki zao, bali Yeye Mwenyewe Amechukua jukumu la kuwapangia kila moja haki yake ili asipatikane na upungufu au dhulma [&hellip;]<\/p>","protected":false},"author":2,"featured_media":9080,"comment_status":"open","ping_status":"closed","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"_acf_changed":false,"give_campaign_id":0,"_bbp_topic_count":0,"_bbp_reply_count":0,"_bbp_total_topic_count":0,"_bbp_total_reply_count":0,"_bbp_voice_count":0,"_bbp_anonymous_reply_count":0,"_bbp_topic_count_hidden":0,"_bbp_reply_count_hidden":0,"_bbp_forum_subforum_count":0,"footnotes":""},"categories":[98],"tags":[],"class_list":["post-4672","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","hentry","category-sehemu-ya-jamii"],"acf":[],"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/4672","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/users\/2"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/comments?post=4672"}],"version-history":[{"count":4,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/4672\/revisions"}],"predecessor-version":[{"id":16317,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/4672\/revisions\/16317"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/media\/9080"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/media?parent=4672"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/categories?post=4672"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/tags?post=4672"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}