{"id":19208,"date":"2023-01-26T08:59:24","date_gmt":"2023-01-26T08:59:24","guid":{"rendered":"https:\/\/uongofu.com\/?p=19208"},"modified":"2023-01-26T10:18:37","modified_gmt":"2023-01-26T10:18:37","slug":"mwaka-wa-huzuni-kufariki-kwa-abu-twalib","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/uongofu.com\/en\/mwaka-wa-huzuni-kufariki-kwa-abu-twalib\/","title":{"rendered":"MWAKA WA HUZUNI KUFARIKI KWA ABU TWALIB"},"content":{"rendered":"<hr \/>\n<p style=\"text-align: center;\"><span style=\"font-size: 18pt; color: #ff6600;\">AR-RAHEEQ AL-MAKHTUM<\/span><\/p>\n<hr \/>\n<p>Kufariki kwa <span style=\"color: #ff6600;\">Abu Twalib:<\/span> Abu Twalib aliugua na hakuishi muda mrefu baada ya hapo. Kikamjia kifo chake. Alifariki mnamo mwezi wa Rajab mwaka wa kumi wa Utume. Ilikuwa ni miezi sita baada ya kutoka katika bonde walilotengwa.\u00a0 Aidha inasemekana: alikufa katika mwezi wa Ramadhani kabla ya kufa kwa Bi <span style=\"color: #ff6600;\">Khadija<\/span> (Radhi za Allah ziwe juu yake) kwa siku tatu?\u201c (1)<\/p>\n<p>Katika hadithi sahihi kutoka kwa <span style=\"color: #ff6600;\">Al-Musaiyab:<\/span> Inasemwa kuwa Abu Twalib akiwa kitandani mahututi, Mtume (<span style=\"color: #008000;\">\ufdfa<\/span>) na hali ya kuwa mbele yake yuko <span style=\"color: #ff6600;\">Abu Jahli<\/span> akasema: <span style=\"color: #0000ff;\">[Ewe ammi yangu, sema: Hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mw\u00e9nyezi Mungu (\ufdfb), tamko ambalo nitakusogeza kwako mbele ya Mwenyezi Mungu (\ufdfb), ]<\/span> <span style=\"color: #ff6600;\">Abu Jahli<\/span> na <span style=\"color: #ff6600;\">Abdillah bin Abu Umayya,<\/span> walikuwa pale wakasema kumwambia: &#8220;Ewe Abu Twalib unaichukia mila ya <span style=\"color: #ff6600;\">Abdul Muttwalib<\/span>? Hawakuacha kuwa wanamsemesha mpaka likawa jambo la mwisho ambalo alilowaambia ni kuwathibitishia kuwa anafuata mila ya &#8216;Abdul Muttwalib. Mtume (<span style=\"color: #008000;\">\ufdfa<\/span>) akasema, \u201dNitakuombea msamaha mpaka Allah Atakapanikataza kufanya hivyo.\u201d<\/p>\n<p>Ndipo Allah (<span style=\"color: #0000ff;\">\ufdfb<\/span>) A\ufb01poshusha aya hii:<\/p>\n<p style=\"text-align: right;\"><span style=\"color: #008000;\">\u0645\u064e\u0627 \u0643\u064e\u0627\u0646\u064e \u0644\u0650\u0644\u0646\u0651\u064e\u0628\u0650\u064a\u0651\u0650 \u0648\u064e\u0671\u0644\u0651\u064e\u0630\u0650\u064a\u0646\u064e \u0621\u064e\u0627\u0645\u064e\u0646\u064f\u0648\u0653\u0627\u0652 \u0623\u064e\u0646 \u064a\u064e\u0633\u06e1\u062a\u064e\u063a\u06e1\u0641\u0650\u0631\u064f\u0648\u0627\u0652 \u0644\u0650\u0644\u06e1\u0645\u064f\u0634\u06e1\u0631\u0650\u0643\u0650\u064a\u0646\u064e \u0648\u064e\u0644\u064e\u0648\u06e1 \u0643\u064e\u0627\u0646\u064f\u0648\u0653\u0627\u0652 \u0623\u064f\u0648\u0652\u0644\u0650\u064a \u0642\u064f\u0631\u06e1\u0628\u064e\u0649\u0670 \u0645\u0650\u0646\u06e2 \u0628\u064e\u0639\u06e1\u062f\u0650 \u0645\u064e\u0627 \u062a\u064e\u0628\u064e\u064a\u0651\u064e\u0646\u064e \u0644\u064e\u0647\u064f\u0645\u06e1 \u0623\u064e\u0646\u0651\u064e\u0647\u064f\u0645\u06e1 \u0623\u064e\u0635\u06e1\u062d\u064e\u0670\u0628\u064f \u0671\u0644\u06e1\u062c\u064e\u062d\u0650\u064a\u0645\u0650<\/span><\/p>\n<p><span style=\"color: #0000ff;\"><em>[ Haimpasii Nabii na wale walio amini kuwatakia msamaha washirikina, ijapo kuwa ni jamaa zao, baada ya kwisha bainika kuwa hao ni watu wa Motoni.]<\/em>\u00a0 (9:113)<\/span><\/p>\n<p>Na ikashuka:<\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><span style=\"color: #008000;\">\u0625\u0650\u0646\u0651\u064e\u0643\u064e \u0644\u064e\u0627 \u062a\u064e\u0647\u06e1\u062f\u0650\u064a \u0645\u064e\u0646\u06e1 \u0623\u064e\u062d\u06e1\u0628\u064e\u0628\u06e1\u062a\u064e \u0648\u064e\u0644\u064e\u0670\u0643\u0650\u0646\u0651\u064e \u0671\u0644\u0644\u0651\u064e\u0647\u064e \u064a\u064e\u0647\u06e1\u062f\u0650\u064a \u0645\u064e\u0646 \u064a\u064e\u0634\u064e\u0627\u0653\u0621\u064f\u06da \u0648\u064e\u0647\u064f\u0648\u064e \u0623\u064e\u0639\u06e1\u0644\u064e\u0645\u064f \u0628\u0650\u0671\u0644\u06e1\u0645\u064f\u0647\u06e1\u062a\u064e\u062f\u0650\u064a\u0646\u064e<\/span><\/p>\n<p><em><span style=\"color: #0000ff;\">[Kwa hakika wewe humwongoi umpendaye, lakini Mwenyezi Mungu humwongoa amtakaye. Na Yeye ndiye anawajua zaidi waongokao.]<\/span><\/em>\u00a0 (28:56) (2)<\/p>\n<p>Hakuna haja ya kuzungumzia zaidi lile ambalo alikuwa akilifanya <span style=\"color: #ff6600;\">Abu Twalib<\/span> katika kumhami Mtume (<span style=\"color: #008000;\">\ufdfa<\/span>) kwani alikuwa kama ngome ambayo Uislam na Waislam walijikinga na mashambulizi ya Makuraishi na wajinga, isipokuwa yeye aliendelea kufuata mila za wazee na babu zake, hakusilimu. Hakufaulu moja kwa moja kwani imepokewa katika hadithi sahih kutoka kwa <span style=\"color: #ff6600;\">Ibn Abbas bin Abdul Muttwalib<\/span> aliwahi kusema kumwambia Mtume (<span style=\"color: #008000;\">\ufdfa<\/span>): \u201dHukuweza kumsaidia ammi yako, ijapokuwa alikuwa akikuhami, akikutetea na akighadhibika kwa ajili yako&#8221;, Mtume (\ufdfa) akasema, <span style=\"color: #0000ff;\">[ Yeye yumo motoni, na kama si mimi angekuwa katika walio chini kabisa motoni. ]<\/span> (3)<\/p>\n<p>Imepokewa kutoka kwa <span style=\"color: #ff6600;\">Abu Saeed Al-Khudryi<\/span> kuwa alimsikia Mtum\u00e9 (\ufdfa)&#8217; akimtaja ammi yake, akasema: [Huenda akanufaika na uombezi wangu siku ya Kiyama, na kwa hivyo akawekwa mahali palipo karibu na kina cha moto, utakao\ufb01kia katika\ufb01mdo za miguu yake ( nguyu). &#8220;(4)<\/p>\n<div>\n<hr \/>\n<\/div>\n<div><span style=\"color: #ff6600;\"><em>1) Katika _marejeo mengine kuna tofauti kubwa, haya tuliyoyaeleza ya tofauti ya kifo cha Bi Khadija na Abu Twalib, ya siku tatu ndio sahihi zaidi. Kwani marejeo mengi yanakubaliana kuwa kifo cha Abu Talib kilitokea baada ya Hisari kwa miezi sita.<\/em><\/span><\/div>\n<div><span style=\"color: #ff6600;\"><em>2) Sahihil Bukhari, Juzuu 1, Uk. 548.<\/em><\/span><\/div>\n<div><span style=\"color: #ff6600;\"><em>3) Sahihil Bukhari, Juzuu 1, Uk. 548. 204<\/em><\/span><\/div>\n<div><span style=\"color: #ff6600;\"><em>4) Ibn Iawzi katika kitabu chake, Talqiyh, Uk. 7 na Rahmatun Lil \u2019ATumin, Juzuu 2, Uk. 164.<\/em><\/span><\/div>\n<div><span style=\"color: #ff6600;\"><em>*) Arrahiq Al-Makhtuum Uk 203-20<\/em><\/span><\/div>\n<hr \/>","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>AR-RAHEEQ AL-MAKHTUM Kufariki kwa Abu Twalib: Abu Twalib aliugua na hakuishi muda mrefu baada ya hapo. Kikamjia kifo chake. Alifariki mnamo mwezi wa Rajab mwaka wa kumi wa Utume. Ilikuwa ni miezi sita baada ya kutoka katika bonde walilotengwa.\u00a0 Aidha inasemekana: alikufa katika mwezi wa Ramadhani kabla ya kufa kwa Bi Khadija (Radhi za Allah [&hellip;]<\/p>","protected":false},"author":2,"featured_media":15476,"comment_status":"closed","ping_status":"closed","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"_acf_changed":false,"give_campaign_id":0,"_bbp_topic_count":0,"_bbp_reply_count":0,"_bbp_total_topic_count":0,"_bbp_total_reply_count":0,"_bbp_voice_count":0,"_bbp_anonymous_reply_count":0,"_bbp_topic_count_hidden":0,"_bbp_reply_count_hidden":0,"_bbp_forum_subforum_count":0,"footnotes":""},"categories":[57],"tags":[],"class_list":["post-19208","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","hentry","category-sera-ya-mtume"],"acf":[],"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/19208","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/users\/2"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/comments?post=19208"}],"version-history":[{"count":3,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/19208\/revisions"}],"predecessor-version":[{"id":19211,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/19208\/revisions\/19211"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/media\/15476"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/media?parent=19208"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/categories?post=19208"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/uongofu.com\/en\/wp-json\/wp\/v2\/tags?post=19208"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}